Sura4

1 Bapendwa, musiamini kila roho, lakini muzichunguze kama zina toka kwa Mungu. Sababu ba nabii bamingi ba bongo balisha tokea mu dunia. 2 Kwa hii mutatambua Roho ya Mungu: kila Roho yenye inaamini kama Yesu Kristo alikuya kwa mwili, ni ya Mungu. 3 Na kila Roho yenye haiamini Yesu haiko ya Mungu. Ni roho ya mupinga-Kristo mwenye mulisikiaka kama atakuya, na sasa alisha kuya mu duniya. 4 Nyie batoto bapendwa, muko ba Mungu, na mulibashinda sababu mwenye iko ndani yenu iko mukubwa kushinda mwenye iko mu duniya. 5 Ni ba duniya; njo maana banasema byenye kuelekea duniya na duniya inabisikia. 6 Shiye ni ba Mungu ; mwenye anayuwa Mungu, anatusikia, mwenye haiko wa Mungu hatatusikie, kwa ile njo tuna tambua roho ya kweli na roho ya udanganyifu. 7 Bapendwa, tupendane shiye kwa shiye sababu mapendo ni ya Mungu na mwenye anapenda, anazaliwa na Mungu na anamuyuwa Mungu. 8 Mwenye hana mapendo, hamuyuwe Mungu, sababu Mungu ni mapendo. 9 Mapendo ya Mungu ilionakana juu yetu sababu Mungu ali tuma Mutoto wake wa pekee kusudi tuishi ju yake. 10 Mapendo ya Mungu ni ivi: shiye hatu ku mupenda lakini ye njo alitupenda na akatuma Mutoto yake sawa sadaka ya kutegetezwa ju ya kutosha zambi zetu. 11 Bapendwa, kama Mungu alitupenda, tupendane shiye kwa shiye. 12 Hakuna mwenye alishakaona Mungu, kama tuna pendana shiye kwa shiye, Mungu iko ndani yetu na mapendo yake inakamilika ndani yetu. 13 Kwa hii, tunayuwa kama tuko ndani yake na yeye iko ndani yetu, sababu alitupatia sehemu ya Roho yake 14 Tuliona na tunahakikisha kama Baba alituma Mutoto wake kama Mwokozi wa duniya. 15 Mwenye atakubali kama Yesu ni Mutoto wa Mungu, Mungu anaishi ndani yake, naye ndani ya Mungu. 16 Tena tuli yuwa na tuliamini ku mapendu ya Mungu kwetu. Mungu ni mapendo na mwenye anaishi ndani ya mapendo, anaikala ndani ya Mungu na Mungu anaikala ndani yake. 17 Kwa sababu ya hii, mapendo hii inakamilika ndani yetu, kusudi tukuwe na tumaini siku ya hukumu, kwa sababu vile iko njo vile tuko ndani ya duniya hii. 18 Ndani ya mapendo hamuna boga, lakini mapendo ya kweli inaondosha boga, sababu boga inaleta hukumu na mwenye kuogopa hakukamilika ndani ya mapendo. 19 Tunapenda sababu Mungu ali tupenda wa kwanza. 20 Kama mutu anasema:«Napenda Mungu» lakini anachukiya ndugu yake, ni musema bongo. Sababu mwenye hapende ndugu yake mwenye anaonaka, atapenda Mungu mwenye haonake. 21 Na amri alitupatia njo hii: kila mwenye anapenda Mungu, apende ndugu yake.