Sura 3

1 Muone mapendo gani Baba anatupatiya, kusudi batuite batoto ya Mungu, na ni vile tuko. Juu ya hii, duniya haituyuwe, sababu haikumuyuwa Baba. 2 Banduku bapendwa, tangiya sasa tuko batoto ya Mungu, gisi tutakuwa haiya julikana bado. Tunayuwa kama wa kati Kristu ataonekana, tutakuwa kama yeye, na tutamuona gisi iko. 3 Na mwenye iko na ile tumaini ya maisha yenye kujengewa juu yake, ajitakase kama vile ye peke ni Mutakatifu . 4 Na mwenye anaendeleya kufanya zambi ana vunja sheriya sababu zambi ni kukosa kweshimiya sheriya. 5 Muna yuwa kama Kristo alionekana ju ya kuvuta zambi zetu, na ndani yake hamuna zambi. 6 Mwenye ana ishi ndani yake hata endeleya kufanya zambi. Na mwenye anaendeleya na zambi aya muonaka wala kumuyuwa. 7 Batoto bapendwa, musiache mutu abapoteze. Mwenye anatenda haki ni mutu wa haki sawa vile Kristo yepeke ni muhaki. 8 Mwenye ku fanya zambi ni wa shetani, sababu shetani ye peke alifanya zambi tangu mwanzo njo mana Mutoto wa Mungu alikuya kusudi aribishe kazi za shetani. 9 Mwenye ana zaliwa na mungu hafanyake zambi, kwa sababu mbego ya Mungu iko ndani yeke . Hataongeza tena kufanya zambi, sababu anazaliwa na Mungu. 10 Kwa ile batoto ya Mungu na bale bashetani bana julikana. Mwenye afanye haki haiko wa Mungu, mwenye hapendi ndugu yake na ye vile vile. 11 Muwone ujumbe yenye mulisikiya tangia mwanzo: tuna pashwa kupendana bamoya kwa bengine. 12 Haiko sawa Kaina mwenye alikwa wa shetani, akawuwa ndugu yake. Tena sababu gani alimuna ? Ju matendo yake ilikuwa ya mubaya , na ya ndungu yake ilikwa ya kweli. 13 Musi shangale bandugu, kama duniya ina tuchukiya. 14 Tuna yuwa kama tunatambuka kifo tuna pata uzima , sababu tu na penda bandugu. Mwenye ana upendo ndani yake ni mufu. 15 Mwenye ata chukiya ndugu yake ni muuwaji. Na muna djuwa kama muwaji hawezi pata uzima wa milele. 16 Tuli juwa mapendo ya kweli sababu Kristo alitowa uzima yake ju yetu, na shiye tuna pashwa kutowa uzima yetu juu ya beingine. 17 Lakini mwenye iko na mali ya duniya , na ana ona ndugu yake mumagumu ana funga roho, bila kumusikiliya uruma, na munagani mapendo ya Mungu ita kwa ndani yake? 18 Batoto yangu bapendwa, tusi tusipende kwa masemo na kwa kinyua, lakini kwa matendo na kweli. 19 Kwa hiyo tuta yuwa kama tuku ndani ya kweli, na tuta akikisha mioyo yetu ndani yake . 20 Sababu kama moyo wetu inatuhukumu, Mungu ni mukubwa kushinda moyo wetu, na anayuwa kila kitu. 21 Bapendwa, kama moyo wetu haituhukumu, tuko na kitumaini kia kweli mbele ya Mungu. 22 Na yote tutalomba , tutaipata kwake , kwa sababu tunachunga amri yake na tunatenda mema mbele yake. 23 Na hii ni amri yake, yenye tunaamini kwa jina ya Mutoto yake Yesu-Kristo, na tupendane wote kama vile ye peke anatupenda. 24 Mwenye anachunga amri ya Mungu, iko ndani yake na Mungu iko ndani yake. Na kwa hii tunayuwa kama iko ndani yetu, kwa Roho yenye alitupatiya.