Sura 2

1 Batoto, ninabandikiya maneno hii kwa sababu musitende zambi. Kama moya kati yenu anatenda zambi, tuko na mutetezi wa kutusemeya kwa Baba, Yesu Kristo Mutu wa haki. 2 Alijifanya sadaka ya zambi yetu na haiko tu juu yetu , lakini juu ya batu bote ba duniya muzima. 3 Na kwa hiyo, tuna tambuwa kama tunamujuwa, tuki chunga amri zake. 4 Mutu akisema: «minamujuwa Mungu», lakini hachunge amri zake ni mwongo na kweli haiko ndani yake. 5 Na mwenye kuchunga maneno yake, kwa kweli ule mutu, upendo wa Mungu utamufanya kuwa mwenye haki. Na kwa hiyo tunajuwa kama tuko ndani yake. 6 Mwenye anasema: niko ndani ya Mungu, anapashwa kutembeya kama vile Yesu Kristo alitembeya. 7 Mupendwa, sibandikiye amri ya mupya, lakinini ile ya zamani, yenye mulipokeyaka toka mwanzo, na amri ya zamani, ni maneno yenye mulisikiyaka. 8 Lakini minabaandikiya amri mupya, ya kweli ndani ya Yesu na ndani yenu. Kwasababu giza inakimbiya na nuru ina tawala. 9 Mwenye atasema kama iko ndani ya nuru na hapendi ndugu yake, iko ndani ya giza mpaka leo. 10 Mwenye kupenda ndugu yake iko ndani ya nuru na hakutakuwa kitu ya kumwangusha. 11 Lakini mwenye anachukiya ndugu yake iko ndani ya giza, na anatembeya ndani ya giza; na hajuwe kwenye anaenda; kwa sababu giza inamufanya kipofu. 12 Batoto yangu bapendwa minabaandikiya kwa sababu zambi zenu zimesamehewa kwa jina yake. 13 Nabaandikiya ba baba kwa sababu munamujuwa ule mwenye iko tangu mwanzo ya duniya. Nabaandikiya biyana kwasabu muna shinda bajambazi. Nabaandikiya batoto badogo kwa sababu muna muyuwa Baba. 14 Nabaandikiya ba baba kwa sababu munamujuwa ule mwenye iko tangu mwanzo ya duniya. Nabaandikiya biyana kwasabu muko na nguvu na neno ya Mungu iko ndani yenu na mulishinda bajambazi. 15 Musipende duniya wala bitu biko ndani ya duniya, kama mutu akipenda duniya upendo wa mungu hauko ndani yake. 16 Kwasabu yote yenye kuwa ndani ya duniya (tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi ya uzima) haitoke kwa Baba lakini inatoka ku duniya. 17 Duniya na tamaa yake bitapita, lakini mwenye kufanya mapenzi ya Mungu ataishi milele. 18 Batoto badogo, ni wakati ya mwisho. Vile mulisikiyaka kama mupinga-Kristo anakuya, sasa bapinga-Kristo bamingi banaonekana. Kwa ile tuna tambuwa kama ni wakati ya mwisho. 19 Balitoka kati yetu, lakini habakukuwa betu. Kama balikuwa betu, bangebakiya na shiye. Lakini, saa balitoka ndani yetu inaonesha kama habiko betu. 20 Lakini nyie mulipakaliwa na ule mwenye iko Mutakatifu, na muna yuwa kweli. 21 Kama nilibaandikiya sikusema kama hamujuwe kweli lakini ni kwa sababu muna yuwa kama hakuna bongo ndani ya kweli. 22 Nani musema bongo, haiko ule mwenye anapinga kama Yesu ni Kristo? Mutu wa vile ni mupinga-Kristo sababu ana kana Baba na Mutoto. 23 Mubenye bana kana Mutoto hakuna mwenye iko na Baba. Mwenye kujuwa Mutoto iko na Baba. 24 Kwenu nyie, byenye mulisikiyaka tangu mwanzo bibakiye ndani yenu. Kama byenye mulisikiyaka bingali ndani yenu, mutabakiya ndani ya Mutoto na ndani ya Baba. 25 Na ahadi yenye alitwachiya ni hii: Uzima ya milele. 26 Nabaandikiya hii maneno kuhusu benye bangetaka kubapoteza. 27 Basi kwenu, upako yenye mulipata inabakiya ndani yenu, na hamuna lazima ya mutu kubafundisha. Lakini, gisi upako yake ina bafundisha byote na ni kweli, haiko bongo, na gisi alibafundisha mubakiye ndani yake. 28 Na sasa batoto bapendwa, mubakiye ndani yake, kwa sababu wakati atakuya tutakuwa na bidii na hatutapata haya mbele yake wakati atarudiya. 29 Kama muna yuwa ni Mutu wa haki, na muyuwe kila mutenda haki anazaliwa naye.