Sura 5

1 Kila mwenye anaamini kama Yesu ni Kristo, anazaliwa na Mungu. Na kila mwenye anapenda Baba, anapenda pia Mutoto mwenye anazaliwa naye. 2 Kwa sababu hii, tunayuwa kama tunapenda batoto ba Mungu: wakati tunapenda Mungu na kutimiza amri yake. 3 Muone mapendo ya Mungu: tuchunge amri yake. Na amri yake haiko nguvu. 4 Kila mwenye anazaliwa na Mungu anashinda duniya. Na hii njo ushindi wa duniya: imani yetu. 5 Ni nani mwenye anashinda duniya? Ni ule mwenye anaamani kama Yesu ni Mutoto wa Mungu. 6 Mwone mwenye alikuya na mayi na damu: Yesu Kristo. Hakukuya na mayi tu, lakini na mayi na damu. 7 Kwa sababu biko batatu benye banashuhudiya. 8 Roho, mayi na damu. Bote batatu banasikilizana. 9 Kama tukaitika ushuhuda ya batu, ushuhuda wa Mungu ni kubwa sana. Kwa sababu Mungu alishuhudiya Mutoto wake. 10 Mwenye kuamini Mutoto wa Mungu iko na ushuhuda ndani yake. Na ule mwenye haamini Mungu anamufanya kuwa muongo, sababu akusadiki ushuhuda wa Mungu ju ya Mutoto wake. 11 Na hii ni ushuhuda: Mungu alitupatia uzima wa milele, na hii uzima iko ndani ya Mutoto wake. 12 Mwenye iko na Mutoto iko na uzima. Mwenye hana Mutoto wa Mungu hana uzima. 13 Nilibandikia hii maneno kusudi muyuwe kama muko na uzima wa milele, kwa nyie benye munaamini jina ya Mutoto wa Mungu. 14 Tena, tazama tumaini yenye tuko nayo mbele yake, kama tunamulomba kitu yote kufwatana na mapenzi yake, anatusikia. 15 Tena, kama tunayuwa anatusikiya, kyote kyenye tunamulomba, tunayuwa kama tu naipata. 16 Kama mutu anaona ndugu yake kutenda zambi yenye hailete kifo, amuombeye, na Mungu atamwokowa. Na semea apa zambi yenye hailete kifo. Kuko zambi yenye inaleta kifo; siseme kama munapashwa kuiombeya. 17 Ku kosa haki yote ni zambi, lakini kuko zambi yenye ailete kifo. 18 Tuna juwa kama yeyote amezaliwa na Mungu hatendake zambi. Lakini mwenye anazaliwa ndani ya Mungu anajichunga safi, na mujanja awezi kumutendeya ubaya. 19 Tunayuwa kama tuko batu ba Mungu na duniya yote inaongozwa na shetani. 20 Lakini tunayuwa kama Mutoto wa Mungu alikuya na alitupatia akili kusudi tuyuwe mwenye iko kweli. Pia, tuko ndani ya mwenye iko kweli, katika Mutoto wake Yesu Kristo. Yeye ni Mungu wa kweli na uzima wa milele. 21 Batoto bapendwa, mujichunge na masanamu.