Sura 8

1 Sasa tuangalie mambo yanayoelekea nyama zinazotolewa kwa kutambikia sanamu za miungu: tunajua kwamba sisi wote tuko na elimu, kama vile munavyozoea kusema. Elimu inamufanya mtu kuwa na kiburi, lakini upendo unawajenga watu katika imani. 2 Kama mtu anajizania kwamba anajua kitu, yeye hakijui hakika sawa vile inavyomupasa kukijua. 3 Lakini yule anayemupenda Mungu, huyu anajulikana naye. 4 Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mmoja peke yake tu. 5 Kuko wale wanaoitwa miungu katika mbingu na katika dunia, na hivi kuko miungu mingi na wabwana wengi. 6 Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mmoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mmoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake. 7 Lakini si watu wote wanaofahamu mambo hayo. Wengi wamezoea kutambikia sanamu za miungu mpaka sasa, wanakula nyama wakizihesabu hakika kuwa za kutambikia sanamu zile. Kwa sababu zamiri yao ni mbovu, wanajisikia kwamba wanajichafua kwa kula chakula kile. 8 Chakula hakitaleta ushirika kati yetu na Mungu. Kama tukiacha kula hatupungukiwi kitu na kama tukikula hatuongezewi kitu. 9 Lakini, muangalie vizuri kusudi uhuru wenu usiangushe wale wanaokuwa zaifu katika imani. 10 Kwa maana kama mtu zaifu katika imani akikuona wewe mwenye elimu unakula katika hekalu la sanamu, si zamiri yake itamusukuma kula vyakula vya kutambikia sanamu? 11 Na hivi kwa sababu ya elimu yako, yule ndugu mwamini zaifu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, atapotea. 12 Kwa kuwakosesha wandugu zenu kama hivi na kuumiza zamiri yao, ni kama vile munamukosea Kristo mwenyewe. 13 Kwa hiyo chakula kikimwangusha ndugu yangu katika zambi, nitajizuiza kula nyama siku zote kusudi nisimwangushe ndugu yangu.