Sura 7

1 Sasa tuangalie mambo yale muliyoniandikia. Ni vizuri mwanaume asioe. 2 Lakini kwa ajili ya kuepuka uasherati inafaa kila mwanaume akuwe na muke wake wa pekee, na kila mwanamuke akuwe na mume wake wa pekee. 3 Mume anapaswa kumutimizia muke wake mapaswa yake, na muke anapaswa kumutimizia mume wake mapaswa yake. 4 Muke hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa mume wake. Vilevile mume hawezi kuamua sawa anavyotaka juu ya mwili wake mwenyewe; kwa sababu ni mwili wa muke wake. 5 Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu. 6 Maneno hayo ninayowaambia si amri, lakini ni ruhusa tu ninayowapa. 7 Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mtu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mmoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile. 8 Na kwa wale wasiooa bado na wajane, ninawaambia kwamba ingekuwa vema waendelee kuishi peke yao kama vile mimi. 9 Lakini kama hawawezi kujizuiza wao wenyewe, basi waoane; kwa maana afazali kuoa kuliko kuwaka tamaa. 10 Kwa wale waliokwisha kuoana, ninatoa amri hii, isiyotoka kwangu, lakini kwa Bwana Mungu: muke hapaswi kuachana na mume wake. 11 Lakini kama muke akiachana na mume wake, asiolewe tena, kama si vile apatane tena na mume wake. Vilevile mume hapaswi kufukuza muke wake. 12 Na kwa wengine, mimi ninawaambia maneno haya, lakini hayatoki kwa Bwana: kama mume mwamini akiwa na muke asiyeamini, naye muke yule akikubali kuishi pamoja naye, asimufukuze. 13 Vilevile kama muke mwamini akiwa na mume asiyeamini, naye mume yule akikubali kuishi pamoja naye, asiachane na mume wake. 14 Kwa maana, mume asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na muke wake. Vilevile muke asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na mume wake mwamini, watoto wao wangehesabiwa kama watoto wa wapagani. 15 Lakini kama mume au muke mupagani akitaka kuachana na mwamini aliyeoana naye, aachane naye. Katika mambo kama hayo, ndugu au dada mwamini yuko huru, kwa maana Mungu amewaita kusudi mukae katika amani. 16 Wewe muke mwamini unaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa mume wako? Au wewe mume mwamini utaweza kujua namna gani kwamba utamwokoa muke wako? 17 Kwa ngambo ingine, kila mtu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote. 18 Ikiwa mtu alitahiriwa mbele ya kuitwa na Mungu, asitafute kufuta kovu la kutahiriwa kwake. Ikiwa alikuwa hajatahiriwa wakati alipoitwa na Mungu, hapaswi kutahiriwa. 19 Kutahiriwa au kutotahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni kutii amri za Mungu. 20 Inafaa kila mtu abaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa na Mungu. 21 Ikiwa ulikuwa mutumwa wakati Mungu alipokuita, usihuzunike. Lakini ikiwa kuna bahati ya kupata uhuru, usiipoteze bure. 22 Kwa maana mutumwa aliyeitwa kuwa wa Bwana, amepewa uhuru na Bwana. Hivi vilevile mtu mwenye uhuru aliyeitwa na Kristo, ni mutumwa wa Kristo. 23 Mumenunuliwa na Mungu kwa bei kali, basi musikuwe tena watumwa wa watu. 24 Wandugu zangu, inafaa kila mtu akae katika ushirika wake na Mungu akibaki sawa alivyokuwa wakati alipoitwa naye. 25 Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mtu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana. 26 Kwa sababu ya taabu ya siku hizi, ninafikiri kwamba ni vizuri mtu akae sawa vile anavyokuwa. 27 Ikiwa umekwisha kuoa, usitafute kuachana na muke wako. 28 Lakini kama ukioa, haufanyi zambi, na kama binti anaolewa, yeye hafanyi zambi vilevile. Lakini wale wanaooana watakuwa na mateso katika maisha yao, na mimi ninataka kuwaonya kusudi muepuke mateso yale. 29 Wandugu zangu, mimi ninataka kusema hivi: wakati uliopangwa unabaki mufupi. Tangu sasa wale waliooa waishi kama vile wasiooa. 30 Wale wanaolia wakuwe kama vile wasiolia. Wale wanaofurahi wakuwe kama vile wasiofurahi. Wale wanaonunua vitu wakuwe kama vile hawana kitu. 31 Wale wanaotumia mali ya dunia hii wakuwe kama vile wasioitumia. Kwa maana dunia hii inakaribia kupita. 32 Ningependa muishi bila masumbuko yoyote. Mtu asiyeoa anashugulikia mambo ya Bwana, anatafuta jinsi ya kumupendeza Bwana. 33 Lakini mtu aliyeoa anasumbukia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kupendeza muke wake. 34 Yeye anashugulikia mambo mawili. Vilevile mwanamuke asiyeolewa au binti anashugulikia mambo ya Bwana. Anajitolea kwa Bwana katika mwili na moyo wake wote. Lakini mwanamuke anayeolewa, anashugulikia mambo ya dunia, anatafuta jinsi ya kumupendeza mume wake. 35 Maneno hayo ninayosema ni kwa faida yenu, wala si kwa kuwafungia njia. Ninataka kuwaonyesha namna ya kuishi sawa inavyofaa, kusudi mupate kumutumikia Bwana pasipo kizuizo chochote. 36 Mtua akiona kwamba hatembeyi vilivyo kuhusu ubikira wake, kama wakati unapita na inapashwa kuwa hivyo, afanye kile anataka, hatendi zambi, aoe ao aolewe. 37 Lakini yule ambaye ana msimamo mkali katika moyo wake bila kusurutishwa, akiwa na uwezo juu ya tamaa yake mwenyewe na hii ameamua katika moyo wake mwenyewe kulinda ubikira wake mwenyewe anafanya vema. 38 Hivyo, mwenye kutoa ubikira wake kwa kuoa ao kuolewa anafanya vema, na yule ambaye hatowi ubikira wake atafanya vema zaidi. 39 Mwanamuke aliye olewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali mzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye ni huru kuolewa na yule anayetaka, lakini sherti ndoa ikuwe ya kikristo. 40 Lakini ingekuwa heri zaidi kama angekaa sawa vile anavyokuwa. Hilo ni shauri langu, nami vilevile ninazani kwamba ninaongozwa na Roho wa Mungu.