Sura 13

1 Hata nikiwa na uwezo wa kusema luga za watu na za wamalaika, lakini kama sina upendo, masemi yangu ni bure kama vile kelele la kengele au matoazi. 2 Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure. 3 Ninaweza vilevile kugawanya mali yangu yote kwa kulisha wamasikini na hata kutoa mwili wangu uunguzwe, lakini kama sina upendo, hakuna faida ninayopata. 4 Upendo unavumilia, ni wenye wema; upendo hauna wivu, upendo haujivuni, na hauna kiburi. 5 Upendo haukosi kuwa na adabu, hautafuti faida yake mwenyewe, haukasiriki upesi, nao hauhesabii mtu ubaya. 6 Upendo haufurahii ubaya, lakini unafurahia ukweli. 7 Upendo hauchoki na mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote na kuvumilia mambo yote. 8 Upendo haukomi hata kidogo. Lakini kutabiri kunatoweka, zawadi ya kusema kwa luga za ajabu inatoweka, na maarifa yanapita. 9 Kwa maana tunafahamu tu mambo machache na kutabiri tu mambo machache. 10 Lakini wakati mambo matimilifu yatakapokuja, yale yasiokuwa matimilifu yatatoweka. 11 Wakati nilipokuwa mtoto, nilisema kama mtoto, niliwaza kama mtoto, nilifikiri kama mtoto. Lakini nilipokuwa mtu mzima niliacha mambo ya kitoto. 12 Kwa maana wakati wa sasa tunaona kama mwenye kuangalia ndani ya kioo kisichoonyesha wazi, lakini wakati utakaokuja tutaona waziwazi. Kwa sasa ninajua tu mambo machache, lakini nyuma nitajua kwa utimilifu kama vile Mungu anavyonijua mimi. 13 Basi sasa, hivi vitu vitatu vinadumu: imani, tumaini na upendo; lakini kinachokuwa kikubwa kuliko hivi vingine ni upendo.