Sura 12

1 Sasa tuangalie mambo yanayoelekea zawadi za Roho Mtakatifu. Wandugu zangu, sitaki mukose kufahamu ukweli wa zawadi hizi. 2 Munajua kwamba wakati mulipokuwa wapagani, mulikuwa mukivutwa na kupotoshwa na sanamu zisizosema. 3 Kwa sababu hii ninataka mufahamu kwamba hakuna mtu ambaye anaongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema: «Yesu alaaniwe, na hakuna mtu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana,”» kama asipoongozwa na Roho Mtakatifu. 4 Kuna zawadi mbalimbali, lakini ni Roho mmoja anayezitoa. 5 Kuna utumishi wa namna mbalimbali, lakini ni Bwana mmoja ndiye wanayemutumikia. 6 Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mmoja anayewezesha watu wote kuzitimiza. 7 Na kwa kila mtu Roho anajifunua kwa faida ya wote. 8 Basi mtu mmoja anapewa na Roho uwezo wa kusema maneno ya hekima, na mwingine uwezo wa kusema maneno ya ufahamu na Roho yule yule. 9 Mwingine anapewa imani na Roho yule yule na mwingine napewa zawadi ya uwezo wa kuponyesha wagonjwa. 10 Mwingine anapewa uwezo wa kufanya miujiza, mwingine zawadi ya kutabiri, na mwingine uwezo wa kutambua roho ya uongo na Roho wa ukweli. Mwingine alipewa uwezo wa kusema luga za ajabu na mwingine uwezo wa kutafsiri luga zile. 11 Ni yule yule Roho mmoja anayetenda mambo hayo yote, akimupa kila mmoja zawadi mbalimbali kama anavyopenda. 12 Kwa maana, Kristo ni kama mwili mmoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mmoja tu. 13 Vilevile sisi wote, Wayuda na Wagriki, watumwa na watu wanaokuwa huru, tumebatizwa kwa Roho mmoja kusudi tukuwe mwili mmoja na sisi wote tumenyweshwa Roho mmoja. 14 Mwili hauundwi na kiungo kimoja tu, lakini na viungo vingi. 15 Kama muguu ungesema: «Kwa sababu mimi si mukono, basi mimi si wa mwili, hata vile haungeacha kuwa kiungo cha mwili. 16 Na kama sikio lingesema: “Kwa sababu mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hata vile halingeacha kuwa kiungo cha mwili. 17 Kama mwili wote ungekuwa jicho, namna gani ungeweza kusikia? Na kama ungekuwa sikio, namna gani ungeweza kunusa? 18 Lakini sasa, Mungu amepanga viungo vya mwili kila kimoja kama ilivyomupendeza. 19 Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili haungekuwa! 20 Kwa hivi sasa kunakuwa viungo vingi lakini mwili ni mmoja. 21 Jicho haliwezi kuuambia mukono: “Sina lazima yako!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu: “Sina lazima yenu!”» 22 Lakini zaidi ya hiyo, viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa zaifu, ndivyo vinavyokuwa vya lazima. 23 Tena viungo vile tunavyozania kwamba havistahili heshima kubwa ndivyo tunavyoheshimu zaidi. Na viungo vinavyokuwa vya haya ndivyo tunavyotunza sana, 24 wakati vile vinavyoheshimiwa havihitaji kitu. Mungu ameunganisha mwili hata akavipatia heshima zaidi viungo vilivyokosa heshima, 25 kusudi kusikuwe mabishano katikati ya viungo vya mwili, lakini vyote visaidiane sawasawa. 26 Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho. 27 Ninyi wote ni mwili wa Kristo, na kila mmoja wenu ni kiungo cha mwili ule. 28 Vilevile Mungu ameweka kwanza mitume katika kanisa; pili manabii na tatu walimu; kisha kunakuwa wale wenye zawadi ya kufanya miujiza, ya kuponyesha wagonjwa, ya kusaidia wengine, ya kuongoza wengine, ya kusema luga za ajabu. 29 Wote si mitume, manabii au walimu. Wote hawana uwezo wa kufanya miujiza, 30 Ao zawadi ya kuponyesha wagonjwa, wa kusema kwa luga za ajabu, au wa kutafsiri. 31 Basi mutamani sana zawadi inayokuwa bora zaidi.