1 Eliashibu kuhani mukubwa alisimama pamoja na bandugu yake, bakuhuni, na bakajenga mulango ya kondoo. Bakaibariki na bakaitia milango; bakaibariki, kuanzia hamea mpaka Hananeli. 2 Batu ya Yeriko balijenga upande ya Eliashibu, ngambo yake Zakuri mutoto wa Imri na ye vile akayanga. 3 Batoto ya Senaa bakajenga mulango ya samaki. Bakaifunyika, na bakatia milango, machuma na makomeo yake. 4 Karibu nabo, Menemothi mutoto wa Uria mufundi wa kutengemeza, Meshulamu mutoto wa Berekia, mutoto wa Meshezabeli; na karibu nabo alikuwa natumika Sadoki mutoto wa Baana; 5 karibu nabo, balikuwa na tumika Balekoï, bale bakubwa habakujishusha kukazi ya Bwana yabo. 6 Yoyada mutoto wa Pasea, Meshulamu mutoto wa Besodeya, balitengeneza mulango ya zamani. Balifunyika na bakatia milango, machuma na makomeo. 7 Pembeni nabo, balikuwa natumika Melatia, Bagabaoni, na Yadoni, Meronathi na batu ya Gabaoni na wa Mispa, benye banatoka fasi ya liwali ya ngambo ya bahali. 8 Karibu nabo palikuwa natumika Uzeili, mutoto wa Hanhaya, umoja wa bafundi wa dhahabu, na ngambo yake alikuwa natumika Hanania moja wa bafundi wa munukata. Nabo baliacha Yelusalema mpaka kibambazi kirefu. 9 Upande yabo kulikuwa Refaya, mutoto wa Huni, kiongozi wa mtaa moja wa Yelusalema. 10 Upande yabo mbele ya nyumba yake Yedaya, mutoto wa Harumafu, na upande yake kulitumika Hatushi, mutoto wa Hashabneya. 11 Kipande kingine kya kibambazi na mnara wa tanuu ilitengenezwa na Malkiya, mutoto wa Harimu, na Hashubu mutoto wa Pahathmoabu. 12 Upande yabo kulikuwa natumika na batoto bake ya banamuke, Shalumu, mutoto wa Hoheshi, kiongozi wa mtaa wa Yelusalema. 13 Hanuni ne benye banaishi Zona balijenga mulango ya bonde. Balijenga, na bakatia milango, chuma na makomeo. Balifanya madhiraa helfu ya kibambazi mpaka mulango ya nyumba ya chakulaya banyama. 14 Malkia, mutoto wa Rekabu, kiongozi wa mtaa wa Beth-hakaremu, alitengeneza mulango nyumba ya nyama. Akajenga na akatia milango, chuma na makomeo. 15 Shalumu, mutoto wa Kolze, kiongozi wa mtaa wa Mispa akatengeneza mulango ya kisima. Akaijenga, akaifunyika na akatia manguzo, chuma na makomeo. Akajenga kibambazi ya birika la Shiloa, karibu na bustaniya Mfalme, mpaka madaraja yenye itashuka kutoka muji wa Davidi. 16 Nyuma yake, Nehemia, mutoto wa Hasbuki, kiongozi wa nusu mtaa wa Beth-suri, alitumika kwa kutengeneza mpaka makabusi ya Daudi, na mpaka birika yenye ilijengwa, na mpaka nyumba ya bashujaa. 17 Kisha yeye, Balawi balitumika, Rehumi, mutoto wa Bani, na pembeni yake, Hashabia, mwenye alikuwa natumika ju ya mtaa yake, kiongozi wa nusu ya mtaa wa keila. 18 Kisha yeye, bandugu yake balitumika, Binue, mutoto wa Henadodi, kiongozi wa nusu wa mtaa wa Keila. 19 Pembeni yake, Ezeri, mutoto wa Yeshua, mukubwa wa Mispa, akatengeneza kipande kya kibambazi, kinangaliana na kupanda kwa ghala ya silaha. 20 KIsha yeye Baruki, mtoto wa Zakaï, alitengeneza kwa bidii kipande kingine pembe mpaka mulango ya ngumba ya Eliashibu, kuhani mukubwa. 21 Kisha yeye Meremothi, mtoto wa Uria, mtoto wa Hakosi, alitengeneza kipande kingine kuanzia mulango ya nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba wa Eliashibu. 22 Kisha yeye, bakuhani balitumika kando kando ya Yelusalema. 23 Kisha bao, Benyamini na Hashubu balitumika mbele ya nyumba yabo. Kisha bao Azaria, mtoto wa Maaseya, mtoto wa Anania, akatumika kando (pembeni) ya nyumba yake. 24 Kisha Binui, mtoto wa Henadadi, akatengeneza kipande kuanzia nyumba ya Azaria mpaka pembe, na mpaka pembeni. 25 Palali, mtoto wa Uzaï, alitumika mbele pembe na upande kubwa yenye inangaliana na nyumba ya Mfalme karibu na wanja ya mabusu. Kisha yeye Pedaya , mtoto wa Panoshi akatumika. 26 Banethini balikala juu ya mulima bakatumika mpaka pembeni ya mulango ya maji, ku mashariki, na kwenye mnara inatoka. 27 Kisha bao, Batekoï bakajenga kwangaliana na mnara kubwa mpaka kibambazi ya mulima. 28 Juu ya mulango ya punda, bakuhani bakatumika kila moja mbele ya nyumba yake. 29 Kisha bao, Sadoki, mtoto wa Imeri akatumika mbele ya nyumba yake. Kisha yeye, Shemaye, - mtoto wa Shekania, mulinzi wa mulango wa mashariki akatumika. 30 Kisha bao, Hanania, mtoto wa Shelemia, na Hanuni mtoto wa sita wa Salafu, balitengeneza kipande ingine ya kibambazi. Kisha bao, Meshulamu, mtoto wa Berekia akatumika mbele ya chumba yake. 31 Kisha yeye, Malkiya, umoja wa bafundi wa dhahabu, akatumika mpaka na nyumba ya Banethini na ya bafanya biashana, kuangaliana na mulango ya Miphkadi, na mpaka chumba cha juu cha pembeni. 32 bafundi wa dhahabu na bafasiya biashara bakatumika katika chumba cha juu cha pemebeni na mulango ya kondoo.