1 Pa kusikiya habari ya maneno hii, wafalme wote wa ngambo ya Yordani, ku mulima na ku bonde, na ngambo yote pembeni ya bahari kubwa, kufika karibu na Lebani, wahivi, wa Amola, wa Kanana wa Felezi, wa Hivi na wa Yabusi, 2 waka ungana pamoja kwa kupikana na Yoshua na Israeli. 3 Wakaaji wa Gabao, ngambo yao, pale balisikia namna Yoshua ali haribu Yeriko na Aï, 4 Wakatumia hila, waka safiri, benye chakula akiba. Waka valisha punda zao magunia ya zamani, na buyu bya vinyo vyenye kutiliwa vilaka, 5 Na viato vya kushonewashonewa, benye kuvaa mavazi ya zamani sana, na chakula chao mikate yakukauka sana na kuvunjikavunjika. 6 Waka fika karibu na Yoshua, mu kambi ya Gilegale, waka mwambiya; pamoja na Israeli wote: tumetoka inchi ya mbali, sasa fanya agano pamoja nasi. 7 Watu wa Israeli waka wajibu awa wa Hivi: pangine munakaa katikati yetu, je tuta fanya agano? 8 Wakamwambiya Yoshua: sisi na watumishi wako. Yoshua aka wambia:ninyi wa nani, na munatoka wapi? 9 Waka mjibu: watumishi wako wanatoka inchi ya mbali, juu ya kavumu ya Bwana Mungu wako; maana tulisikiya habari yake, kwa yote alifanya mu Misri, 10 Namna ali watendea wafalme wawili wa Amola ile ngambo ya Yordani, Siho, mfalme wa Hesboni, na Ogi, mfalme wa Basani alikuwa Asitaroti. 11 Na wazee wetu pamoja na wakaji wa inchi yetu wali tu ambiya: chukuweni chakula ya safari na mufike mbele yao, na mutawambiya: sisi ni watumishi wenu, fanyeni sasa agano na sisi. 12 Ona mkate wetu: ilikuwa ya moto pale tuli itwala ingali moto nyumbani mwetu, siku tuli ondoka kuya mbele yenu, sasa inakauka na kuvunjikavunjika. 13 Na vibuyu vyetu vya vinyo, tulivijaza vingali vipya, sasa vinapasuka; mavazi yetu na viato vina arabika juu ya safari ndefu 14 Watu wa Israeli waka chukuwa chakula yao na hawakutafuta shauri kwa Bwana. 15 Yoshua aka fanya amani nao, na kupatana agano juu ya kuwa acha wazima, na viongozi vya mkutano waka wa apia. 16 Siku tatu kisha kufanya agano, watoto wa Israeli wakasikia kwamba ni majirani wao, na wanakaa katikati yao. 17 Maana watot wa Israeli wakaenda, na kufika kwa muji wao siku ya tatu; muji yabo ni Gabao, kafira, Beroti na kirija Yearimi. 18 Ha wakuwapika, juu viongozi vya mkutano wali wa apia mbele ya Bwana Mungu wa Israeli, kuwa acha wazima. Lakini mkutano mzima wakanungunikia viongozi. 19 Na viongozi waka ambiya mkutano: tuli wa apia mbele ya Bwana Mungu wa Israeli, sasa hatuwezi kuwagusa. 20 Ona vile tuta watendeya: tuta wa acha wazima, hasira ya Mungu isije juu yetu, sababu ya kiapo tuli wa fania. 21 Viongozi waka wambia: watabaki wazima. Lakini wa kuwa na kazi ya kukata nkuni na kushota maji juu ya mkutano wote, vile viongozi wali wambiya. 22 Yoshua aka waita na kusema nao hivi; kwa nini mulitudanganya, kusema: tuko wa mbali sana, kumbe muko naishi katikati yatu? 23 Muna laaniwa sasa, na muta kuwa kwenye utumwa ya sipo kwisha, kuta kuni na kushota maji ku nyumba ya Mungu wangu. 24 Waka mjibu Yoshua, kusema: poali twambiya sis wa tumishi wako ma agizo ya Bwana, Mungu wako, kwa Musa, mtumishi wake, kumitolea inchi yote na kuwangamiza wakaji wote mbele yenu, na kufika yenu inatuletea oga sana juu ya uzima yetu, njo kwa maana tulifanya namna hii. 25 Sasa sisi ni mikononi mwako, ututendee vile itakupendeza kutenda. 26 Yoshua aka watendea vile alipanga, aka waokowa mikononi mwa watoto wa Israeli, benye haba kubauwa. 27 Lakini aka wafanya kuwa wenye kukata kuni na kushota maji juu ya mkutano, na juu ya mazababu ya Bwana pahali Bwana ataji chakulia: wanafanya kazi ile mpaka leo.