SURA 7

Watoto wa Israeli waka tenda zambi juu ya vitu vyenye ku laaniwa. Akan, mtoto wa kalami, mtoto wa Zabidi, Mtoto wa Zeraki, wa kizazi kya Yuda aka chukuwa vitu vilivyo kataliwa. Na kasirani ya Bwana ika wakia watoto wa Israeli. 2 Yoshua akatuma toka Yeriko watu kwenda Aï, iko karibu na Bet-Aveni, ku magaribi mwa Beteli. Aka wa ambiya: mupande, na mupeleze inchi. Na, wakapanda na kupeleleza Aï. 3 Wakarudi kwake Yoshua, naku mwambia: hakuna faida kutembeza taifa yote; elfu mbili ao tatu ya watu itatosha kushamulia Aï; usi wachoshe watu, ju wako wadogo. 4 Karibu na watu elfu tatu wakaenda, lakini waka kimbiya mbele ya watu wa Aï. 5 Watu wa Aï waka uwa karibu na watu makumi tatu na sita; waka wakimbiza kwanza mulango kufika shebarimu, waka wapika pa mutelemuko. Taifa ikafazaika na kupoteza bidii. 6 Yoshua akapasua na vazi yaka, na akapika goti uso chini mpaka magaribi, mbele ya sanduku ya Bwana, yeye na wazee wa Israeli, na wajitia majifu kichwani. Yoshua akasema: 7 Eh, Bwana Mungu , kwa nini uli wapitisha Yordano taifa hii, juu uttoe mikononi mwa ba Amola nakutu uwisha? Ee, tunge bakia ile ngambo ya Yordani. 8 Ee, Bwana tasema nini, kisha Israeli kukimbiya mbele ya adui zake? 9 Bakanana pamoja na wakaaji wa inchi wataisikiya, wata tuzunguka, na watafuta jina yetu mu dunia. Nawe, utafanya nini juu ya Jina lako? 10 Bwana aka ambiya Yoshua: Simama! kwa nini unabakia kulala uso chini? 11 Israeli ana fanya kosa; wana vunja agano yangu nili wa agiza, wana kamata ku vita vya kulaniwa na vyenye kukataliwa, walivi iba na kuyaficha ndani ya mizigo. 12 Kwa iyo wana wa Israeli hawa wezi kusimama mbele ya adui zabo, wata kimbiya kwa sababu wana laaniwa. Sita kuwa tena nanyi, kama ha mutii sheriya yangu. 13 Simama, takasa taifa. Utawa ambiya: mujitakase kwa kesho; maana Bwana anasema, Mungu wa Israeli; kuna uchafu katikati yako, Israeli; hautaweza kusimama mbele ya adui mpaka mutajitakasa 14 Mutanikaribia asubui kizazi kwa kizaei. Na kizazi yenye Bwana ata taya kitakaribia jamaa kwa jamaa, na jamaa yenye Bwana atataja, itakaribia nyumba kwa nyumba; na nyumba yenye Bwana ata taja ikaribia mutu kwa mutu. 15 Mwenye atatajiwa kama yeye alibeba kitu kya laana tachomwa, yeye na vitu vyake vyote, kwa maana alivunja agano la Bwana na kutenda maovu katika Israeli. 16 Yoshua aka amuka asubui sana, na kukaribisha Israeli kizazi kwa kizazi, na kizazi cha Yuda kika tajiwa. 17 Aka karibisha ma jamaa ya Yuda, na jamaa ya Zeraki ika tajiwa. aka karibisha jamaa Zeraki ile nyumba kwa nyumba, na Zabidi ikatajiwa. 18 Nyumba ya Zabidi ika karibishwa mutu moja moja, na Akana, mtoto wa Kalami, mtoto wa Zabidi; mtoto wa Zeraki, wa kizazi ya Yuda, akatajiwa. 19 Yoshua aka ambia Akano: mtoto yangu, usifu Bwana, Mungu na Israeli, umuabudu uni ambiye nini ulifanya, usinifiche kitu. 20 Akana aka mujibu Yoshua, na kusema: Ni kweli natenda zambi mbele ya Bwana Mungu wa Israeli na kinye nilifanya ni hiki. 21 Nili ona kati ya nyara koto mzuri ya inchi ya shinea sikeli ya feza mia mbili na kilo moja ya zahabu; nili vitamani, na nika vikamata; vina fichiwa mu udongo, chini ya hema yangu, na feza iko juu. 22 Yoshua akatuma batu, bakakimbilia ku hema na tazama, vitu vilifichwa ndani ya hema ya Akana, na feza yulu. 23 Wakabikamata, naku bileta mbele ya Yoshua na watoto wa Israeli wote, nakubipeleka mbele ya Bwana. 24 Yoshua pamoja na Israeli wote, wakamukamata Akana, mtoto wa Zeraki, koti, na ile kilo moja ya zahabu, batoto ya Akana bote, ma ngombe yake , na mpunda na makondoo yake, hema yake na kila kitu kyake, naku batelemusha mu bonde la Akole. 25 Yoshua akasema: kwa nini unatuvuruka hivi? Bwana naye atakuhangaisha leo. Na Israeli wote waka mupika majiwe. Waka wachoma kwa moto wakawapika majiwe. 26 Waka simamisha yulu yake majiwe wengi sana yenye inabakia mpakaleo. Na Bwana aka shusha kasirani yake. Njo maana, juu ya jambo ile, fasi ikaitwa bonde la Akole.