1 Yerico ilifungiwa na kutiliwa vizwizi mbele ya watoto wa Israeli. Haku kuwa mutu wa kutoka na wa kwingiya. 2 Bwana aka mwambiya Yosua: hona, na ipana Yeriko na mfalma wake pamoja na maaskari washudia wake mu mikono yako. 3 Zunguluka inje ya mugini, mwebote wapikanaji wote, muizunguke mara moja. Uta fanya ivi kwa siku sita. 4 Makuhani saba wata beba mbele ya sanduku ya sanduku baragumu; saba yenye kuliya sana; siku ya saba, muta izunguka mugini mara saba; na makuhani watapika baragumu. 5 Wakati watapika ile pembe ya kuliya nguvu sana, wakati mutasikiya kulia kwa baragumu, taifa yote itapika kelele nguvu. Pale, ukuta wa muji ita anguka, na watu wote wata panda, kila mutu mbele yake. 6 Yosua, mtoto wa Nuni, akaita ma kuhani, na aka wa ambiya: bebeni sanduku la agani, na makuhani saba wa chukuwe baragumu ya kulia sana mbele ya sanduku la Bwana. 7 Na aka ambiya batu: tembeyeni, mu izunguke mugini, na watu wenye silaha wapite mbele ya sunduku za agano ya Bwana. 8 Wakati Yosua ali ongeya na batu, makuhani saba benye kubeba mbele ya Bwana baragumu saba ya kulia sana, wa anja kwenda na kupika baragumu. Sanduku ya agano ya Bwana ili bafwata nyuma. 9 Batu benye silaha balitembeya mbele ya makuhani benye kupika baragumu, na kundi ili tembeya na kupika baragumu. 10 Yosua ali agiza watu: musi pike kelele, sauti yenu isi sikilike, na kinwa yenu isiseme neno kufika siku ntaba ambiya: pikeni kelele! pale mutapika kelele. 11 Sanduku ya Bwana ikazunguka muji, ikafanya mara moya kwa siku, kasha bakarudia kambi, na bakapitisha usiku pale. Yosua aka lamuka asubui sana, na makuhani waka beba sanduku ya Bwana. 12 Yosua aka lamuka asubui sana na makuhani waka beba sanduku ya Bwana. 13 Makuhani saba wenye kubeba baragumu saba yakulia sana mbele ya sanduku ya Bwana waka anza kutembeya na kupika baragumu. Wenye silaha wali enda mbele yao, na kikundi kilifwata sanduku la agano; mu kutembeya, wakapika baragumu. 14 Bakazunguka muji mara moya, siku ya pili; kisha bakarudiya ku kambi. Waka ifanya vile siku sita. 15 Siku ya saba, wakalamuka asubuyi sana, mapambazuko, na bakafanya namuna ila tu njo bali zunguka mara saba kwa muji. 16 Kwa mara ya saba, vile makuhani wali kuwa wanapika baragumu, Yosua akambiya batu: bikeni kelele, maana Bwana anamitolea muji! 17 Muji italaaniwa na Bwana, muji na yote iko ndani yayo; lakini muta acha buzima kwa Lehaba ule ndumba na bale bote batakuwa ndani ya nyumba yake juu alifuchika mijumbe tuli tumaka. 18 Mujichunge sana kwa kitu kya kulaaniwa, maana muki chukuwa kinye muna laani, muta tia kambi la Israeli mu laana mutaleta vuruko. 19 Feza yote na zaabu yote, vyongo vyote vya chuma na vya shaba vitakuwa takatifu juu ya Bwana, vita ingizwa kati ya akiba la Bwana. 20 Taifa ikapika kelele, na makuhani bakapika baragumu, wakati watu walisikia sauti ya baragumu baka pika kelele ya nguvu sana, na kibambasi ika anguka, watu watu waka panda mu muji, kila moja mbele yake. Baka bamba muji. 21 Na wakaharibu byenye kulahaniwa byote kwa upanga. Waka uwa kila kitu mu muji, bana ume na bana muke. Batoto na bazee, kufika ku ngombe, ma kondoo na mapunda. 22 Yosua aka baambiya bale batu bawili bali peleleza inchi: ingiyeni mu nyumba ya ule mwana muke ndumba, na tosheni ule mwana muke na batu yake bote, vile muli mulapiya (mulaka). 23 Ba biyana, bapelelezi, bakaingiya, nakumutosha Lehaba, bayake, mama yake, banduku yake na bote balikuwa naye; bakatosha bote ba jamaa yake, nabaka weka pembeni ya kambi ya Israeli. 24 Baka choma muji na byote bilikuwa ndani; lakini wakaweka ndani ya akiba ya nyumba ya Bwana, feza, zahabu, na byombo byote bya chuma na shaba. 25 Yesua akaacha uzima kwa lehaba ule ndumba, kwa nyumba ya baba yake, na kwa bale bote bali kuya pamoja naye; akaikala mu katikati ya Israeli mpaka leo, ju alifuchika wa jumbe wale Yosua alitumaka ku peleleza Yeriko. 26 Njo pale Yosua aka lapa na kusema: ala aniwe mbele ya Bwana mutu ule atasimama nakujenga upia hii muji wa Yeriko! atajenga msingi palufu ya mtoto wake wa kwanza, na atasimisha milango palufu lwa kitenda mimba wake. 27 Bwana akakuwa na Yoshua, na kavumu yake ikajulikana mu inchi yote.