1 Ephraimu anakula pepo, na anafata pepo ya mashiriki; kila siku anazidisha bongo na uharibifu akafanya masikilizano pamoya na Asuria, naba kabeba mafuta ku Egypitu. 2 Bwana naye alikwa na mapingano na Yuda, na akalipiza ya kobo dju ya kutembeya yake, aka murusishia sawa sawa na matendo yake. 3 Dani ya tumbo yakobo aligusa ndugu yake kusigino, na ku nguvu yake, pamoya na Mungu alikwa na uwezo. 4 Pamoja na malaika, na aka shinda, akalia, na aka musihi. Yakobo alimukuta ku Betelemu, na kule njo, Mungu akatusemea. 5 Bwana ni Mungu wa majeshi; jina yake ni Bwana. 6 Na weye, rudilia Mungu wako, shunga wuma wa uhaki, na tegemea tu Mungu wako. 7 Ephraimu ni muchuruzi mwenye iko na kipimo mubaya ku mikono , anapenda ku dangania. 8 Ephraimu anasema: kwa ukweli, mina kwa tajiri mina pata mali, Lakini ni malipo ya kazi yangu yote, habataono ndani yangu zambi ndio uovu. 9 Na miye, niko Bwana,Mungu wako, wa inchi ya Egypitu; nda kuikalisha tena chini ya hema, sawa ku masiku ya feti. 10 Nambiya ba nabii, na ongeza maono, na kupitia ba nabii nimetumia mifano. 11 Kama Galadi niyabure, batakwa kweli babure bata toa toa zabichu ya ngombe ku Gilgali: na mazabahu yabo ita kwa kame mafungu ndani ya matuta ya sshamba. 12 Yakobo akambia ku inchi ya Aramu, Israeli akatumikiya dju ya ku pata mwana muke, na dju yaku pata mwanamuke akachunga kondoo. 13 Kwa nabii moya Bwana akapondisha Israeli inje ya Egypitu, na kwa nabii moya Israeli aka chungiwa. 14 Ephraimu aka sirikisha Bwana sana: Bwana aka mutupilia damu yenye alimwanga, aka murudishia laumu yake.