Ng'ombe saba wembamba waliwala wale ng'ombe saba wanene.
Masuke saba membamba yalimeza yale masuke saba mema.
Waganga na wenye hekima wa Farao hawakuweza kutafsiri ndoto za Farao.
Mkuu wa wanyweshaji alimwambia Farao ya kwamba kijana wa Kiebrania alitafsiri kwa usahihi na ndoto ya mwenzake walipokuwa kifungoni.
Yusufu alisema ya kwamba Mungu angejibu ndoto ya Farao na upendeleo.
Yusufu alisema ya kwamba Mungu alikuwa akitamka kwa Farao kile Mungu alichotaka kufanya.
Wale ng'ombe saba wema na masuke saba mema yaliwakilisha miaka saba ya mema.
Wale ng'ombe saba wembamba na masuke saba membamba yaliwakilisha miaka saba ya njaa.
Farao alipewa ndoto mbili kwa sababu suala lilikuwa limethibitishwa na Mungu, na Mungu angetekeleza hivi karibuni.
Yusufu alimshauri Farao kuchagua mtu kukusanya moja ya tano ya mazao katika miaka saba ya mema.
Farao alisema ya kwamba Roho ya Mungu ilikuwa ndani ya Yusufu.
Farao alimpatia Yusufu mamlaka juu ya nyumba ya Farao na juu ya nchi yote ya Misri, wa pili tu kwa Farao.
Yusufu alitunza mazao kama mchanga wa bahari, kiasi kisichohesabika.
Wana wa Yusufu walikuwa Manase na Efraimu.
Miaka saba ya njaa ilikuwa katika nchi yote.
Yusufu alifungua maghala yote na kuuza chakula kwa Wamisri wote.
Dunia yote ilikuja Misri kununua mazao kutoka kwa Yusufu.