Genesis 41

Genesis 41:4

Katika ndoto ya kwanza ya Farao, ng'ombe saba wembamba na ng'ombe saba wanene walifanya nini?

Ng'ombe saba wembamba waliwala wale ng'ombe saba wanene.

Genesis 41:7

Katika ndoto ya pili ya Farao, masuke saba membamba yalifanya nini kwa masuke saba mema?

Masuke saba membamba yalimeza yale masuke saba mema.

Waganga na wenye hekima wa Farao walitafsirije ndoto zake?

Waganga na wenye hekima wa Farao hawakuweza kutafsiri ndoto za Farao.

Genesis 41:12

Mkuu wa wanyweshaji alimwambia nini Farao kuhusu Yusufu?

Mkuu wa wanyweshaji alimwambia Farao ya kwamba kijana wa Kiebrania alitafsiri kwa usahihi na ndoto ya mwenzake walipokuwa kifungoni.

Genesis 41:14

Yusufu alisema ni nani angetafsiri ndoto ya Farao?

Yusufu alisema ya kwamba Mungu angejibu ndoto ya Farao na upendeleo.

Genesis 41:25

Yusufu alisema ya kuwa Mungu alikuwa akitamka nini kwa Farao?

Yusufu alisema ya kwamba Mungu alikuwa akitamka kwa Farao kile Mungu alichotaka kufanya.

Wale ng'ombe saba wema na masuke saba mema yaliwakilisha nini ndani ya ndoto?

Wale ng'ombe saba wema na masuke saba mema yaliwakilisha miaka saba ya mema.

Genesis 41:27

Wale ng'ombe saba nyembamba na masuke saba membamba yaliwakilisha nini ndani ya ndoto?

Wale ng'ombe saba wembamba na masuke saba membamba yaliwakilisha miaka saba ya njaa.

Genesis 41:30

Kulingana na Yusufu, kwa nini Farao alipewa ndoto mbili?

Farao alipewa ndoto mbili kwa sababu suala lilikuwa limethibitishwa na Mungu, na Mungu angetekeleza hivi karibuni.

Genesis 41:33

Yusufu alimshauri Farao kuchukua katika miaka saba ya mema sehemu ipi ya mazao ya Misri?

Yusufu alimshauri Farao kuchagua mtu kukusanya moja ya tano ya mazao katika miaka saba ya mema.

Genesis 41:37

Farao alisema nini imo ndani ya Yusufu?

Farao alisema ya kwamba Roho ya Mungu ilikuwa ndani ya Yusufu.

Genesis 41:39

Farao alimpatia Yusufu nafasi gani ya mamlaka?

Farao alimpatia Yusufu mamlaka juu ya nyumba ya Farao na juu ya nchi yote ya Misri, wa pili tu kwa Farao.

Genesis 41:48

Yusufu alitunza kiasi gani cha mazao katika miaka saba ya mema?

Yusufu alitunza mazao kama mchanga wa bahari, kiasi kisichohesabika.

Genesis 41:50

Wana wawili wa Yusufu waliozaliwa kabla ya njaa walikuwa kina nani?

Wana wa Yusufu walikuwa Manase na Efraimu.

Genesis 41:53

Miaka saba ya njaa ilisambaa kiasi gani?

Miaka saba ya njaa ilikuwa katika nchi yote.

Genesis 41:55

Yusufu alifanya nini watu wa Misri walipomlilia Farao kwa ajili ya chakula?

Yusufu alifungua maghala yote na kuuza chakula kwa Wamisri wote.

Ni nani alikuja Misri kununua mazao kwa Yusufu?

Dunia yote ilikuja Misri kununua mazao kutoka kwa Yusufu.