Genesis 42

Genesis 42:1

Yakobo alimtuma nani Misri kununua mazao?

Ndugu kumi wa Yusufu, bila Benyamini, walikwenda Misri kununua mazao.

Genesis 42:5

Ndugu wa Yusufu walifanya nini walipokuja kwa Yusufu kununua mazao?

Ndugu wa Yusufu waliinama chini kwake nyuso zao kuelekea ardhini.

Genesis 42:7

Yusufu alifanya nini alipowagundua ndugu zake.

Yusufu alijibadili na kuongea kwa ukali na ndugu zake.

Genesis 42:9

Yusufu alitoa mashtaka gani dhidi ya ndugu zake?

Yusufu aliwashtaki ndugu zake kuwa wapelelezi.

Genesis 42:12

Ndugu zake Yusufu walisema ndugu wao mdogo yupo wapi?

Ndugu zake Yusufu walisema ndugu yao mdogo alikuwa na baba yao katika nchi ya Kaanani.

Ndugu zake Yusufu walisema ndugu yao aliyepotea yupo wapi?

Ndugu zake Yusufu walisema ndugu yao aliyepotea hakuwa hai tena.

Genesis 42:14

Yusufu aliwapa ndugu zake mtihani gani kudhihirisha hawakuwa wapelelezi?

Yusufu alisema ndugu zake hawataondoka Misri, hadi pale ndugu yao mdogo aje Misri.

Yusufu aliwaweka ndugu zake wapi na kwa muda gani?

Yusufu aliwaweka ndugu zake kifungoni kwa siku tatu.

Genesis 42:18

Yusufu aliwaambia ndugu kufanya nini ili waweze kuishi?

Yusufu aliwaambia kuruhusu mmoja wa ndugu kuwekwa gerezani, wakati wengine wakichukua mazao hadi Kaanani na kumleta ndugu yao mdogo.

Genesis 42:21

Kwa nini ndugu zake Yusufu waliamini matatizo haya yalikuja juu yao?

Waliamini ya kwamba damu ya Yusufu ilidaiwa kwao kwa kile walichofanya kwa Yusufu.

Genesis 42:23

Yusufu alifanya nini aliposikia ndugu zake wakizungumza kuhusu kile walichofanya kwake?

Yusufu aliposikia ndugu zake wakizungumza kuhusu kile walichofanya kwake, Yusufu akatoka kwao na kulia.

Yusufu alirudisha nini ndani ya magunia ya kila ndugu?

Yusufu alirudihsa pesa ya kila ndugu ndani ya gunia lake.

Genesis 42:26

Ndugu walichukuliaje walipogundua ya kuwa kila gunia la ndugu lilikuwa na pesa ndani mwake?

Mioyo yao ilizimia na wakasemeshana kati yao wakitetemeka.

Ndugu walimlaumu nani kwa matatizo yao ya muda huo?

Ndugu walimlaumu Mungu, wakiuliza kwa nini Mungu alifanya hivi kwao.

Genesis 42:35

Ndugu na Yakobo waligundua nini walipotoa kila kitu ndani ya magunia?

Waligundua ya kwamba pesa ya kila mtu ilikuwa ndani ya gunia lake.

Yakobo aliogopa kitu gani kutokea kwa sababu ya suala lao?

Yakobo aliogopa ya kwamba Simoni na Benyamini watachukuliwa kutoka kwake.

Genesis 42:37

Rubeni alitoa kiapo gani kwa Yakobo?

Rubeni aliapa kumrudisha benyamini kwa Yakobo kutoka Misri; la sivyo watoto wawili wa Rubeni wanaweza kuuwawa.

Je Yakobo alimruhusu Rubeni kumpeleka Benyamni Misri?

Hapana, Yakobo hakumruhusu Rubeni kumpeleka Benyamini Misri.

Yakobo alisema nini kingetokea kwake kama Benyamni angekufa?

Yakobo alisema ya kuwa angeshuka na majonzi kaburini kama Benyamini angekufa.