Aliwaweka gerezani kwa sababu walimkasirisha.
Mnyweshaji na mwokaji kila mmoja aliota ndoto usiku huo huo.
Wote wawili walikuwa na huzuni kwa sababu hakuna aliyeweza kutafsiri ndoto zao.
Yusufu alisema ya kwamba Mungu angeweza kutoa tafsiri ya ndoto zile.
Yusufu alisema ya kwamba ndoto ilimaanisha kuwa ndani ya siku tatu Farao atarejesha mnyweshaji katika shughuli yake.
Yusufu aliomba ya kwamba mnyweshaji amkumbuke, na kumtaja kwa Farao, na kumtoa nje ya gereza.
Yusufu alisema ya kwamba ndoto ilimaanisha katika siku tatu Farao atamtundika mwokaji juu ya mti.
Siku ya kuzaliwa ya Farao ilikuwa siku tatu baadae.
Farao alimrejesha mnyweshaji, lakini alimtundika mwokaji, kama Yusufu alivyotafsiri kwao.
Hapana, mnyweshaji hakukumbuka kumsaidia Yusufu, lakini alimsahau.