Genesis 22

Genesis 22:1

Ni mtihani upi Mungu alimpatia Abrahamu?

Mungu alimwambia Abrahamu kwenda katika nchi ya Moria na kumtoa Isaka kama sadaka ya kuteketezwa.

Abrahamu aliitikiaje kwa amri ya Mungu

Abrahamu aliamka asubuhi na mapema na kuanza safari yake katika mahali Mungu alipomwambia.

Genesis 22:4

Abrahamu aliwaambia nini vijana wake wawili ya kuwa yeye na Isaka walikwenda kufanya nini?

Abrahamu aliwaambia vijana wake wawili ya kwamba yeye na Isaka walikwenda kuabudu na kisha wangerudi.

Genesis 22:7

Isaka alimuuliza swali gani Abrahamu walipokuwa wakitembea pamoja?

Isaka alimuuliza Abrahamu, "Yuko wapi mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?"

Abrahamu alijibuje swali la Isaka?

Abrahamu alisema ya kwamba Mungu mwenyewe angetoa mwanakondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketeza.

Genesis 22:9

Walipofika mahali pale, Abrahamu aliaanda nii kama sadaka ya kuteketezwa na alifanyaje?

Abrahamu alimuandaa Isaka kama sadaka wa kuteketezwa kwa kumfunga na kumlaza juu ya madhabahu.

Genesis 22:11

Abrahamu alipochukua kisu mkononi mwake, malaika wa Yahwe alimwambia nini Abrahamu?

Malaika wa Yahwe alimwambia Abrahamu kutomdhuru Isaka.

Malaika alisema alijua nini kuhusu Abrahamu?

Malaika alisema ya kwamba alijua ya kuwa Abrahamu alimcha Mungu.

Genesis 22:13

Mungu alitoaje sadaka wa kuteketezwa kwa ajili ya Abrahamu?

Kulikuwa na kondoo dume amenaswa katika vichaka nyuma ya Abrahamu, ambaye Abrahamu alimtumia kama sadaka wa kuteketezwa.

Abrahamu alipaitaje mahali pale pa sadaka ya kuteketezwa?

Abrahamu alipaita mahali pale, "Yahwe atatoa"

Genesis 22:15

Malaika alitoa sababu gani ya kumbariki Abrahamu?

Malaika wa Yahwe alimwambia angembariki Abrahamu kwa sababu Abrahamu hakujizuia mwanawe wa pekee.

Genesis 22:18

Ni kupitia kwa nani na kwa nini mataifa yote ya dunia yatabarikiwa?

Kupitia uzao wa Abrahamu mataifa yote ya dunia yatabarikiwa, kwa sababu Abrahamu alimtii malaika wa sauti ya Yahwe.