Genesis 23

Genesis 23:1

Abrahamu alifanya nini kwanza Sara alipokufa?

Sara alipokufa, Abrahamu aliomboleza kwanza kwa ajili yake na akamlilia.

Genesis 23:3

Abrahamu alitoa ombi gani kwa wana wa Hethi?

Abrahamu aliomba mali ya kutumia kama sehemu ya kuzikia.

Genesis 23:5

Wana wa Hethi walijibuje ombi la Abrahamu?

Wana wa Hethi walimpatia Abrahamu makaburi bora ya kwao.

Genesis 23:10

Abrahamu alipoomba pango la Efroni Mhiti, Efroni aliitikiaje?

Efroni alijitolea kumpatia Abrahamu pango na shamba kando yake.

Genesis 23:12

Abrahamu aliitikiaje kuhusu ahadi ya Efroni?

Abrahamu alijitolea kulipia shamba pamoja na pango.

Genesis 23:14

Abrahamu aliitikiaje kuhusu ahadi ya Efroni?

Efroni aliomba shekeli mia nne za fedha kwa ajili ya shamba na pango.

Mazungumzo kati ya Abrahamu na Efroni yalimalizikaje?

Abrahamu alilipa shekeli mia nne za fedha kwa Efroni kwa ajili ya sehemu ile ya shamba.

Genesis 23:17

Nini kilikuwa ndani ya manunuzi wa shamba la Efroni ambalo lilikuwa Makpela?

Shamba, pango lililokuwa ndani mwake, na miti yote iliyokuwa katika shamba na mpakani ilijumuishwa katika manunuzi ya Abrahamu wa shamba la Efroni.

Genesis 23:19

Abrahamu baadae alifanya nini na pango?

Abrahamu baadae alimzika Sara katika pango.