Genesis 21

Genesis 21:1

Yahwe alifanya nini kwa ajili ya Sara?

Yahwe alimtembelea Sara naye akazaa mtoto kwa Abrahamu katika muda alioahidi.

Isaka alipokuwa na umri wa siku nane, Abrahamu alifanya nini?

Isaka alipokuwa na umri wa siku nane, Abrahamu alimtahiri.

Genesis 21:5

Sara alisema Mungu amemfanya atende nini?

Sara alisema ya kwamba Mungu alimfanya acheke.

Genesis 21:8

Katika siku Isaka alipoachishwa kunyonya, Sara aliona nini?

Sara alimuona mtoto wa Hajiri akimdhihaki.

Genesis 21:10

Sara alimwambia Abrahamu afanye nini na Hajiri na mwanawe, na kwa nini?

Sara alimwambia Abrahamu kuwafukuza hajiri na mwanawe, kwa sababu mtoto wa hajiri asingeweza kuwa mrithi pamoja na Isaka.

Mwitikio wa Abrahamu kwa dai la Sara ulikuaje?

Abrahamu alihuzunishwa kwa dai la Sara.

Genesis 21:12

Mungu alimwambia Abrahamu afanye nini?

Mungu alimwambia Abrahamu kumsikiliza Sara.

Genesis 21:14

Hajiri na mwanawe walikwenda wapi baada ya Abrahamu kuwafukuza?

Hajiri na mwanawe walikwenda katika jangwa.

Genesis 21:17

Mungu alimwambi Hajiri angemfanyia nini mtoto wake?

Mungu alisema angemfanya mwanawe Hajiri kuwa taifa kubwa.

Genesis 21:19

Hajiri na mwanawe waliponaje?

Mungu alifungua macho ya Hajiri naye akaona kisima cha maji.

Nini kilitokea kwa mtoto wa Hajiri alipokuwa akikua?

Mtoto wa Hajiri akawa mwindaji na mama yake akampatia mke kwa ajili yake kutoka Misri.

Genesis 21:22

Abimeleki alimtaka Abrahamu kuapa kufanya nini kwake?

Abimeleki alimtaka Abrahamu kuapa ya kwamba hatamfanyia baya Abimeleki, au watoto wake, au uzao wake. Abimeleki alimuomba Abrahamu kuonyesha kwake agano lile lile la uaminifu ambalo Abimeleki alikwisha muonesha Abrahamu.

Genesis 21:25

Abrahamu alilalamika juu ya nini kwa Abimeleki?

Abrahamu alilalamika kwa Abimeleki juu ya kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikichukua kutoka kwake.

Genesis 21:28

Kwa nini Abrahamu alituma kondoo wa kike saba kwa Abimeleki?

Abrahamu alituma kondoo saba wa kike kwa Abimeleki kama ushahidi ya kwamba alichimba kisima chenye malumbano.

Genesis 21:31

Abimeleki alirudi katika nchi gani?

Abimeleki alirudi katika nchi ya Wafilisti.

Genesis 21:33

Abrahamu alifanya nini katika mti wa mkwaju katika Beerisheba?

Abrahamu alimwabudu tahwe, Mungu wa milele.

Abrahamu aliishi wapi kwa siku nyingi?

Abrahamu aliishi katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.