1
Mukuye seke ba bana mufatirisha Mungu; sa batoto bapendwa;
2
Na mutembeye dani ya mapendo, kwa mufano ya Kristo, ule ari tupenda , na ari ritowa ye moya kwa Mungu djo yetu sa sadaka na matolewo ya arufu muzuri.
3
Bucharati , kushikuye butshafu iyi namuna , na taama , ishi taiwa ata katchikatchi yenu, djo vile ina pasha kwa batakatifu.
4
Bashi shikiye wala misemon ya sho eshima , wala mitshezo ya bubumbafu, wala mamitshezo , bintu biko kinyume ku buzuri ; tushi kiye matendo ya shukrani.
5
Kwamana , mudjuwe muzuri , busharati ata bumoya , wala butshafu , wala taama , ni ku sema , wa kwabudu , ayina na uriti mu bufalme ya Kristo na ya Mungu.
6
Muntu ashi mi lande kupitiya ma misemo ya sho mana; kwamana ni djo ya bile bintu makari ya Mungu ita anguka kwa batoto ya butomboji.
7
Mushikuye seke na semu na mweye.
8
Murikuya ngiza zamani , na sasa muko mwangaza dani ya Bwana. Mutembeye sa vile batoto ya mwangaza!
9
Kwamana ma tunda ya mwangaza ina elekewa mu buzuri yote ya kila namuna, ya aki na ya ukweri.
10
Tshunguza ile iko muzuri kwa Bwana ;
11
Na mushi riunge ku matendo mubaya ya ngiza, lakini mu yi ukumu.
12
Kwamana ina leta aya ya kusema bile beko na fanya muku futchama;
13
Lakini bile biote bina ukumiwa ina onekana kupitiya mwangaza , kwamana bile biote bina rionesha ni mwangaza.
14
Ni dju ya vile iriendikiwa : lamuka , weye uko na lala , lamuka weye mu bafu, na Kristo ana kwangaza.
15
Mwepuke kuritebesha na ekima , apana kama vile ba bumbafu , lakini sa vile bantu ya akiri;
16
mu uze wakati , kwamana mashiku iko mubaya.
17
Ni djo mana mushi kuye ba sho beyi , lakini mushikiye ni nini mapenzi ya Bwana.
18
mushi lewe vinio : ni bucharati. mukuye , kwanza , benye ku djaziwa na Roho Mutakatifu ;
19
mu patane kupitiya ma zaburi , mamimbo , na kupitiya mimbo ya kiroho , mu imbe na kushukuru na roho yenu yote matukuzo ya Bwana;
20
Murudishi kila wakati neema dju ya bintu biote kwa Mungu Baba, mu djina ya Bwana wetu Yesu-Kristo,
21
Mu rishushe ba moya kwa bengi dani ya Boka bwa Kristo.
22
Mwana muke , muti ba bwana yenu , sa vile kwa Bwana;
23
Kwamana Bwana ni chefu wa mwana muke, sa vile Kristo ni chefu ya kanisa, ile ni mwili yake , na ile eko Mukombozi.
24
kwa lakini , sa vile kanisa ina ti kwa Kristo, bana muke nabo bana pasha kuya vile kwa ba bwanabo mu bintu biote.
25
Bwana , mupede ba bibiyenu , sa vile Kristo ana penda kanisa, na kuri peleka yemo dju yayo ,
26
Djo ya kutakasa kupitiya neno , kisha ku itakasa kupitiya ubatizo ya mayi,
27
Djo ya ku onesha bele yake ile kanisa utukufu , pashipo butshafu , wala zagila , wala pashipo kufana nisha, lakini butakatifu na shaba.
28
Ni djo vile babwana panapasha kupenda ba bibi yabo sa vile mwili yabo . Ule ana penda bibi yake ana ripenda ye moya.
29
Kwamana akuna muntu atezi ku tchukiya mwili yake ; lakini ana irishaka na ku itengeneza ,sa vile Kristo ana fanyaka dju ya kanisa,
30
djo tuko bipande ya mwile yake.
31
Djo kwamana mwanaume ata atcha baba na mama yake , na kuriunga kwa bibi yake , na bo bawiri batakuya mwili moya.
32
Iyi Siri iko munene ; mina sema dju ya Kristo na ya kanisa.
33
Mu kinyume , muntu wote katiyenu a pende bibi yake sa vile ye moya, na bibi a echimiye bwana yake.