1
Batoto , mushikiye bazazi yenu , vile Bwana , kwamana ile iko aki ,
2
Echimiya baba yako na mama yako ( ni embri ya kwanza na malako) ,
3
Djo ukuye na furah na u ishi mwaka mingi pa dunia.
4
Na mweye , ba baba , mushi tshokoze batoto yenu , lakini mu ba fudishi mu ku batengeneza na mu ku ba fudisha mwa Bwana.
5
Bafanya kazi , mweshimiye ba kubwa benu mu ki mwili , na boka na kutetemeka, mu ku rishusha ya roho yenu, sa vile kwa Kristo,
6
Apana paka bele yabo , sa vile kufuraisha bantu, lakini sa vile ba fanya kaji ya Kristo , banafanya na roho muzuri mapenzi ya Mungu.
7
Mu ba tumikiye na roho yote , sa vile munatumikiya Bwana na apana bantu,
8
Muyuwe asema mutu wote , akuye mutumwa , wala uru , atapata kwa Bwana mu ile ata fanya ya muzuri.
9
Na muye , bakubwa , mu fanya na mweye vile kwabo, na mu epuke fudjo , mu djuwe asema mukubwa wabo na wenu eko mu bingu, na kumbele yake akuna butchakuzi ya bantu.
10
Kwa ina bakiya , Muri kabule nguvu mwa Bwana , na kupitiya nguvu yake uwezo yote .
11
Mu vale ma sila yote ya Mungu , djo mu shimame imara ku bukalamushi ya shetani.
12
Kwamana a tuna apa dju ya ku kombana na mwili na damu , kwalakini ni na matawala , na uongozi , na bariti ya iyi dunia ya ginza, na ma pempo ya makari mu mafashi ya yulu.
13
ni vile , mubebe ma sila ya Mungu , djo ya kushimama mu machiku ya mubaya , na kuchimama imara kisha kutambuka.
14
Muchimame seke imara : mukuye na ukweri kama muchipi mukivuno yenu; muvale gambo ya aki;
15
Muvale dju ya bilato kumikulu yenu mabao ile ina leta engili ya salama ;
16
Mubebe yulu ya biote ukingo ya imani, na ile mutezi kujima ma djiya yote ya moto ya mukalamushi;
17
Mubebe tena chapo ya kokolewa , na mupanga ya kiroho , ile ni neno ya Mungu.
18
Mufanye mu wakati yo kupitiya roho mahombi ya namuna yote na ya buluma . muchimame ku ile na kwedeleya beleyote , na muhombe djo ya batakatifu bote.
19
Muhombe djo yangu , dju ni pewe , pale mitafungula kinya , ya kudjuwisha vile inapasha na uru siri ya engili ,
20
Djo ya ile niko mushimamizi dani ya bifungo , na ile mina sema na kwakikisha sa vile mina pasha mu kusema
21
Dju na mweye , muyuwe ile ina nyangariria , iyi ni na fanya , Tychike , mupendwa nduku na mukamilifu na mwaziri dani ya Bwana , ata mionesha biote.
22
Mina mutuma biyobiyo kwenu , djo mu yuwe ali yetu , na djo a poleshe ma roho yenu.
23
Salama na mapendo na imani imi pewe ku banduku kutoka kwa Mungu Baba na kwa Bwana Yesu - Kristo!
24
Neema ikuye na na mwebote muna pemda Bwana Yesu - Kristo kwa mapendo ya mushimamo.