1 Batu ya Galilaya balimuambia kama Pilato alichanga damu na ile ya sadaka yabo. 2 Yesu akibaambia tena «Munawaza kama bale bagalilaya balipta batu bote na zambi ku benye biko ku galilaya juu ya mateso enye bana ona vile? 3 Apana, vile vile kama amupende kutubu muta teswa ginsi baliteswa. 4 Oho batu kumi na munane ya silowa benye mnara ili baangukiaka küsha balikufaka mu na waza kama balishinda batu yote ya Yerusalemu ku zambi? 5 Apana, nabaambia «kama amuache zambi muta teswa nyiye bote.» 6 Yesu alibaezea fumbo ihi «Mutu moja alipanda muti ya muzabibu alikuya kutafuta muzabibu mbegu hakuipata. 7 Mutu akamuambia mulimaji, angalia inakuwa myaka tatu niko nakuya ku tafuta mbengu laki sikute, ukale ile muti juu aina faida ya kuikala kushamba bure bila faida. 8 Mulimaja aka mujibia «uhiache mwaka ihi ntachimbula pembeni ya mizizi nitatia mboleo. 9 Kama itazala mbeku mwaka kesho itakuwa muzuri, uta ikala kama itakala kuzala!» 10 Siku ya sabata Yesu alikuwana fundisha ndani ya shirika. 11 Kulikuwa mwanamuke moja alikuwa na mizimu akukuwa na nguvu ya kusimama juu mukongo yake ilikuwa ya kukunjama. 12 Wakati Yesu alimuona akisema «Mwanamuke uzaifu wako inafunguliwa. 13 13Ilimutia mikono maramoja akanyoloka pia aka tukuza Mungu. 14 14Lakini kiongozi wa shirika akufurai juu Yesu ana ponyesha mutu siku ya sabato, kushi waongozi akaelezea batu «kuko siku sita inaomba kutumika muna weza kuja kujiponye apana siku ya sabato» 15 Bwana akamuambia «Uku mnafiki nani kati yenu afungulake ngombe yake, mbuzi ao kondoio yzake bila kui peleka ku mutoni juu ikunywe mai siku ya sabato?» 16 Njoo mahana uyu muke ni mutoto wa Abrama mwenye sheta alifufunga myaka kumi na munane myaka mingi aweze kufunguliwa siku ya sabato? 17 Wakati alikuwa na sema vile, bale balikuwa na musimama waka sikia aya, njoo batu bote balifurai sana na iyomambo enye ilitukuza Mungu. 18 Kumbi Yesu akasema «Ufalme wa Mungu itapinganishwa na nini? ao itafananishwa na nini? 19 Ufalme wa Mungu inafanishwa na mbengu ya mutarda enye mutu anapanda ku shamba yake, iliota na ikakuwa mutu kubwa, njoo ndeke za hangani inakuja kujenga ka mitawe yahe. 20 Akisema tena «Nitafanisha na nini ufalme wa Mungu? 21 Inafana na dawa ya mikate iyi mwanamuke ali changishaka na kopo tatu ya bunga ya mikate küsha ina vimba» 22 Yesu alitembea na kuhubiri kila mungina na kijiji yote enye ilikuwa ku njia ya yerusalema. 23 Na mutu moja akamuliza «Bwana ni batu chache bata akoka ?» Yesu akamujibu: 24 «Ujikase kuingiya ku mulango mwembamba, bengi bata penda na abata weza kuingia.» 25 Wakati mwenye nyumba atasimama na kufunga mulango, kumbi ngiye muta bakia inje, muta kokola ku mulango mutasema «Bwana, Bwana utufungulie tuingiye» ata jibu mare moja. «Sibajuwe munatoka wapi?» 26 Joo muta sema«tulikula na kunywa pembeni yako tena uli ubiri ku balabala yetu.» 27 Hita bajibia «kusema sibajuwe, munatota wapi, mutoke pembeni yangu muko batenda mobaya.» 28 Kilio itakuwa nakusanga meno wakati mutaona Abalahama, Issaka, Yakobo na ba nabihi biko ndani ya ufalme wa Mungu, lakini bata batupa inje. 29 Bata kuya ngambo ya mashikiri, kusimi, kasikazi pia magaribi bata kuwa kumeza ndani ya ufalme wa Mungu. 30 Na mujuwe batu ya kwaza batakua ba mwisho ba mwisho bata kuwa bakwanza. 31 Bafarisayo balikuya pole pole ku muambia «Toka hapa wende sababu Herode iko na penda kuku uwa.» 32 Yesu akabajibia «muelizee ile muswera; sasaivi niko na fukuza mizimu na kuponesha batu leo pia kesho siku ya tatu nitafika mwisho. 33 Ku iyi maneno yote iko muzuri niendelee na kazi leo, kesho siku ijaa abaweze ku uwa nabihi inje ya Yerusalema. 34 Yerusaleme, Yerusaleme! Weye uko piga majiwe na kuvwa ma nabihi benye niko na kutumia, mara ngapi nalipenda kuchanganisha batoto yako ginsi kuhu ina changa batoto chini ya mabawa yake lakini aupende. 35 Angalia nyumba yako inaachuwa; nakuambia auta mona tena mpaka mutasema "ubarikiwe ule mulenye iko na kuya kujina ya Bwana"