Sura 5

1 Basi, munisikilize sasa ninyi watajiri! Mulie na kuomboleza kwa sababu ya taabu itakayowapata. 2 Mali yenu imeoza, na nguo zenu zimekuliwa na nondo. 3 Zahabu na feza yenu vimepata kutu. Na kutu hii ndiyo itakayowashitaki, nayo itateketeza mwili wenu kama vile moto. Mumejiwekea akiba katika siku hizi za mwisho. 4 Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo! 5 Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa. 6 Mumewahukumu na kuwaua wenye haki, nao hawakupingana nanyi. 7 Basi wandugu, muvumilie mpaka Bwana atakaporudia. Muangalie namna mulimaji anavyongojea shamba litoe mavuno yanayokuwa ya faida kubwa. Yeye anavumilia mpaka wakati mvua ya kwanza na ya mwisho zinaponyesha. 8 Nanyi vilevile, muvumilie na kutia mioyo yenu nguvu, kwa maana Bwana yuko karibu kurudi. 9 Wandugu zangu, musinungunikiane ninyi kwa ninyi kusudi Mungu asiwahukumu. Muangalie, mwamuzi ni karibu, naye amekuwa kwenye mulango! 10 Wandugu zangu, mukumbuke manabii waliotabiri kwa jina la Bwana, muangalie namna walivyovumilia katika mateso, nanyi mufuate mufano wao. 11 Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema. 12 Lakini zaidi ya yote, wandugu zangu, musiape! Musiape kwa jina la mbingu, wala kwa jina la dunia, wala kwa jina la kitu kingine chochote. Museme Ndiyo ikiwa munataka kusema ndiyo. Nanyi museme Hapana ikiwa munataka kusema hapana, kusudi musihukumiwe na Mungu. 13 Kati yenu kuna mtu anayekuwa katika mateso? Aombe kwa Mungu. Au kuna mtu anayekuwa katika furaha? Aimbe nyimbo za sifa. 14 Kati yenu kuna mugonjwa? Awaite wazee wa kanisa, nao watamwombea wakimupakaa mafuta kwa jina la Bwana. 15 Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa. 16 Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa. 17 Elia alikuwa mtu kama sisi. Yeye aliomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya inchi kwa muda wa miaka mitatu na nusu. 18 Kisha akaomba tena, na mbingu ikanyesha mvua, na inchi ikatoa mazao yake. 19 Wandugu zangu, mtu mmoja kati yenu akipotea mbali na ukweli, na mtu mwingine akimurudisha, 20 mukumbuke neno hili: yule anayemurudisha mwenye zambi toka njia ya upotevu ataokoa roho ya yule kutoka kifo, na zambi nyingi zitasamehewa.