Sura 1

1 Yenye ilikuwa kumwanzo (yenye tulisikia tuliona na macho yetu, tuliangalia, na mikono yetu iligusa) kuhusu neno la uzima. 2 Na uzima yenye ilionekana, na tuliona, na tu naishuhudiya, tunabatangaziya maisha ya milele, yenye ilikuwa na Baba, na ilionyeshewa kwetu. 3 Yenye tuliona na tulisikia, tu na baambia pia, ju mushirikiane na siye. Na ushirika yenu iko pamoya na Baba, na Mutoto wake Yesu Kristo. 4 Tuta baandikia hii maneno kusudi furaha yetu ikuwe muzuri kabisa. 5 Hiyi njo habari tulisikia kutoka kwake na tunabatangaziya: Mungu ni nuru na hakuna hata giza kwake. 6 Tukisema kama tunashirikiana naye na tunatembea mu giza, tunadanganya na hatuseme kweli. 7 Lakini tukitembea ndani ya nuru kama vile yeye iko ndani ya nuru, tukonashirikiana bamoya kwa bengine. 8 Tukisema hatuna zambi, tuna jidanganya, na hakuna kweli ndani yetu. 9 Lakini kama tukitubu zambi yetu yeye ni muaminifu na wa haki ju ya kutusamehe na kutusafisha na mabaya yote. 10 Na tukisema kama hatukufanya zambi, tunamufanya mwongo, na neno yake haiko dani yetu.