Sura 1

1 Yuda, mutumishi wa Yesu Kristo, na ndugu wa Yakobo, kwa bale banaitwa bapendwa kwa Mungu Baba, na kuchungwa sababu ya Yesu Kristo. 2 Rehema, amani na mupendo yake iongezeke kwenu. 3 Wapendua, nilijikaza sana kwa kubandikiya juu wokovu ya wote. Nilipashwa kubaandikiya kusudi mufanye vita ya kweli juu ya imani yenye baamini balipewa mara moya. 4 Kwa sababu batu mingi balijiingiza kati yenu kwa uficho. Ni batu benye balichaguliwa sababu ya kuhumu. Benye abaamini nehema ya Mungu na banaidilisha na mambo ya mwili, nabanakatala Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. 5 Sasa, napenda kubakumbusha, (hata kama muliiyuwa yote) kama Bwana aliokowa batu kitoka Ejipito(Misri), Yuma ya ile aliaribisha benye habakuamini. 6 Tena na ba malaika benye habakuchunga utukufu wabo lakini bakaacha makao yabo (Mungu alibachunga katika kifungo kya milele, ndani ya giza, sababu ya hukumu ya siku kubwa). 7 Ni sawa Sodoma na Gomora na miji jirani wakajitowa wenyewe kwa uzinifu na wakafuata tamaa yasio kawaida. Walikamatwa kuwa mufano kwa wote weko nateswa na moto wa milele. 8 Namuna moya, wale wenye kulota kuaribisha miili yao, wanatupa mamlaka na kusema bitu bisiyo na maana juu ya viumbe vya utukufu. 9 Hata malaika mukubwa Mikaeli wakati alimupinga shetani na kugombaniya mwili ya Musa, hakuweza kusema mabaya juu yake. Lakini alimwambia: «Bwana akuhukumu mwenyewe !» 10 Lakini wale watu, wanatukana byenye habayuwe. Na byenye banashikiya (hata wanyama wasiyokuwa na akili wanayuwa). Ni ile inawaharibu. 11 Ole kwao ! kwa sababu wanatembea mu njia ya Kaina na wanajitupa mu makosa ya Balaamu ju ya faida yake. Waliharibika ndani ya kuasi ya Korea. 12 Hawa ni vikwazo katika ma feti yenu ya mapendo. Wanasherekeya bila haya, na wakikula tu kwa kujifurahisha. Ni mawingu bila mayi, yenye kupeperushwa. Ni miti bila matunda (inakufua mara mbili, inangolewa). 13 Ni zoruba kali ya bahari, inaongeza haya yao, ni nyota yenye kuwayawaya na giza ya milele inatayarishwa kwa ajili yao. 14 Enoki wa saba mu kizazi ya Adamu, alitabiri na kusema: «Angalia, Bwana anakuya na ma elfu na elfu ya watakatifu wake. 15 Anakuya kwa kutimiza hukumu juu ya dunia yote. Anakuya kushinda wabaya wote, sababu ya matendo yao yote ya bure ile wenye zambi wasio amini waliosema juu yake.» 16 Ni watu wana nungunika na kulialiaya, wakakimbiya tamaa zao mubaya. Ni wenye kiburi, juu yaa faida zao, wara kudanganya wengine. 17 Lakini, wapendwa, mukumbukeni maneno ilisemewa zamani kupitiya mitume wa Bwana Yesu Kristo. Wali waambia: 18 «Wakati wa mwisho, kutakuwa wenye kuzarau, wenye watafata tamaa zao za mwili.» 19 Hawa watu, wanaleta ubaguzi. Ni wa dunia na hawana Roho. 20 Lakini ninyi wapendwa, mujijenge ninyi wenyewe katika imani takatifu na muombe kupitiya Roho Mutakatifu. 21 Kaeni katika upendo wa Mungu na muchunge rehema ya Bwana yenye kumileteya uzima wa milele. 22 Muwe wenye rehema kati ya wale weko na mashaka. 23 Muwaokowe wengine kwa kuwatosha mu moto. Kwa wengine, muwe na rehema pamoya na woga. Muchukiye hata mavazi yenye kuchafuliwa na mwili. 24 Sasa, kwa ule anayeweza kumilinda katika kuanguka na kumitembeza bila kosa na furaha kubwa mbele ya utukufu wake, 25 Kwake pekee, Mungu wa Mwokozi wetu, kupitiya Yesu Kristo Bwana wetu: utukufu, heshima, utawala na uwezo iwe kwake, jana, leo na milele. Amina.