1 Yabini mufalme wa Hastori, kisha kusikia mambo hii, akatuma wajumbe kua Yobabu mufalme wa Madoni, kua mufalme wa Shimaroni, kua mufalme wa Akishafa. 2 Kwa mufalme wale walikuwa kaskazini ndani ya mulima, ndani kiwandja ya kusini kati ya kinnerti, ndani ya bonde, na juu milima ya Dori, kule kusini. 3 Kwa wakanani wa mashariki na wa magaribi, wa Amola, wa hiti, wa Ferezi, wa Yebusi mu milima, na Hivi chini ya Hermoni ndani ya inchi ya Mispa. 4 Wakatoka, wao na majeshi yao wote pamoja na wao, wana fanya watu wasipo hesabwa sawa kichanga ile iko pembeni ya bahari, na walikuwa na ma punda na ma gari kbwa ya mingi sana. 5 Wafalme waka chaguwa fazi ya masungumuza, na wakatembea pamoja karibu ya maji ya Meroni, juu ya kupiga Israeli vita. 6 Bwana aka mwambiya Yoshua: musiwaogope, kwa maana kisho, kwa hii wakati, nita watowa wote waisha kupigwa na Israeli. 7 Yoshua, pamoja na wapiganaji wake wote wakafika mara moja juu yao karibu na maji ya Meromi, na waka kimbilia mu katikati yao. 8 Bwana aka watowa mu mikono ya Israelu; waka wapiga na kuwa fwatiliya mupaka Sidoni mukubwa, mupaka Miselefoti-Maïmi, na mupaka bonde ya Mitspa kuenda mashariki; waka wapiga, bila kuacha mumoja wao kukimbia. 9 Yoshua aka watendea sawa Bwana limuambia; akakata lishipa ya migeni ya mapunda, na akalunguza ma gari yao. 10 Kwa kuridi kwake, na kwa wakati ile ile, Yoshua akakamata Hatsori, na akapiga mufalme kwa upanga: Hatsori ilikuwa wakati ingine muji mukuu ya ufalme ule wote. 11 Wakapiga wa upanga na waka aribisha wote walipatikana kule, aku kubaki kitu kyole kilikuwa na pumuzi, na waka lunguza Hatsori. 12 Yoshua aka kamata migini yote na wafalme wao wote, na aka wapiga kwa ukali ya upanga, na aka wakaribisha wote sawa sawa na vile Musa mutumishi wa Mungu. 13 Lakini Israeli hakulunguza ata migini ile ilikuwa juu ya milima, ila tu ya Hatsori, ililunguzwa na Yoshua. 14 Watoto wa Israeli waka chunga juu yao, nyara ya ile migini na wanyama; lakini wakapiga kwa ukali ya upanga watu wote, mupaka wali waharibu, bila kuacha kio kiote kilikuwa na pumuzi. 15 Yoshua aka timiza maagizo ya Bwana kwa Musa, mutumishi wake, na toka Musa kwa Yoshua; bila ku acha ata neno moja kutoka yote ile Bwana aliagiza Musa. 16 Ndjo hivi Yoshua alikamata inchi yote, ya mulima, ya kusini, ya inchi yote ya Goseni, ya bonde, ya kiwanja, ya mulima ya Israeli na ya mabonde yaka. 17 Tangu mulima wazi ile inakuya juu ya Seïla mpaka baali-Gadi, ndani ya bonde ya Libani, chini ya miguu ya mulima ya Hermoni. Waka kamata wafalme wao wote, waka wapiga wa kuwa uwa. 18 Vita ya Yoshua na wale wafalme wote ili kawiya sana. 19 Hakukuwa ata muji ilipata amani pamoja na watoto wa Israeli, ili tu Gabaoni, wa Hivi waliketi kule; wakaikamata miji yote kua kugombana. 20 Kwa maana Bwana aka wapa watu kichwa nguvu ya kupambana na watoto wa Israeli, ili Israeli waharibu wote bila ku acha kitu, pasipo kuya na rehema juu yao, na kuwaharibu, sawasawa Bwana alimuagiza Musa. 21 Mwa ile wakati, Yoshua akaanza mwendo, na akamaliza wana Anaki baku mulima ya Hebeloni ya Debiti, ya Anabu, wa mulima yote ya Yuda na ya mulima wote ya Israeli; Yoshua aliwaharibu wote, pamoja na migini yao. 22 Aku kubakiya watoto wa Anaki ndani ya inchi ya watoto wa Israeli; walibaki paka ku Gaza, na ku Gata na mu Asdodi. 23 Yoshua akaivamia inchi yote, ku fwatana na ile Bwana aliambia Musa. Na Yoshua akawapa kwa uriti Israeli, kila mutu sehemu yaka, kufatana na bizazi. Kisha, inchi ika pumuzika na pasipo vita.