Sura 18

1 Baada ya haya Daudi akawashambulia Wafilisti na kuwashinda. Alichukuwa Gathi na vijiji vyake katika utawala wa Wafilisti. 2 Kisha akamshinda Moabu, na Wamoabu wakawa watumishi wa Daudi na wakamlipa ushuru maalumu. 3 Daudi kisha akamshinda Hadadezeri, mfalme wa Zoba huko Hamathi, wakati Hadadezeri alipo kuwa akisafiri kuimarisha utawala wake kwa Mto wa Frati. 4 Daudi akateka magari ya farasi elfu, wanaume wa farasi elfu saba, na wanajeshi wa miguu elfu ishirini. Daudi aliwajeruhi farasi wote wagari, lakini akahifadhi baadhi kwa ajili ya magari ya farasi mia moja. 5 Wakati Waaramia wa Damasko walipo kuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Zoba, Daudi aliua wanaume elfu ishirini na mbili wa Kiaramia. 6 Kisha Daudi akaweka vikosi huko Aramu ya Damasko, na Waaramia wakawa watumishi wake na wakamletea ushuru maalaumu. Yahweh alimpatia Daudi ushindi popote alipoenda. 7 Daudi alichukua ngao za dhahabu zilizo kuwa kwa watumishi wa Hadadezeri na kuleta Yerusalemu. 8 Kutoka Teba na Kuni, miji ya Hadadezeri, Daudi alichukuwa shaba nyingi sana. Ilikuwa shaba hii ambayo baadae Sulemani alifanya beseni ya shaba, iitwayo "bahari", nguzo na vifaa vya shaba. 9 Wakati Toi, mfalme wa Hamathi, aliposikia kuwa Daudi ameshinda majeshi yote ya Hadadezeri mfalme wa Zoba, 10 Toi akamtuma Hadoramu mwanae kwa Mfalme Daudi kumsalimia na kumbariki. Alifanya hili kwa sababu Daudi alipigana na Hadadezeri na kumshinda, na kwa sababu mara nyingi Toi alikuwa kwenye vita naHadadezeri. Toi pia alimtumia Daudi vyombo vya aina mbalimbali dhahabu, na fedha, na shaba. 11 Mfalme Daudi alivitenga vitu hivi kwa Yahweh, pamoja na fedha na dhahabu aliyo ibeba kutoka kwa mataifa yote: Edomu, Moabu, watu wa Amoni, Wafilisti, na Waamaleki. 12 Abishai mwana wa Zeruia akawaua Waedomi elfu kumi na nane katika Bonde la Chumvi. 13 Alieka vikosi huko Edomu, na Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi. Yahweh alimpa Daudi ushindi pote alipoenda. 14 Daudi alitawala Israeli yote, na alitoa haki na uadilifu kwa watu wote. 15 Yoabu mwana wa Zeruia alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mtunza kumbukumbu. 16 Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Shavisha alikuwa mwandishi. 17 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa kiongozi wa Wakerethi na Wapelethi, na wana wa Daudi walikuwa maofisa wakuu mkononi mwa mfalme.