Yusufu alilia kwa sauti alipojidhihirisha kwa ndugu zake.
Ndugu hawakuweza kumjibu Yusufu kwa maana walikuwa wameshtushwa.
Mungu alimtuma Yusufu Misri kuhifadhi uhai, na kutunza familia yake kama msalia wa duniani.
Mungu alimfanya Yusufu baba kwa Farao, bwana wa nyumba yote ya Farao, na mtawala juu ya nchi yote ya Misri.
Yusufu aliambia familia yake kuja na kuishi katika nchi ya Gosheni ambapo angewapa mahitaji.
Yusufu aliwaambia ndugu zake kuharakisha na kumleta baba yake Misri.
Farao alipendezwa sana, na akamwambia Yusufu kuwaambia ndugu zake kumleta baba yao na nyumba zao kuishi katika nchi nzuri ya Misri.
Benyamini alipokea vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha, na Israeli alipokea punda ishirini ya punda waliobeba bidhaa.
Moyo wa Israeli ulishikwa na mshangao, kwa maana hakuamini ndugu walipomwambia.
Israeli alisema alitaka kumuona Yusufu kabla hajafa.