Genesis 45

Genesis 45:1

Yusufu alifanya nini alipojidhihirisha kwa ndugu zake, ambacho Wamisri walisikia?

Yusufu alilia kwa sauti alipojidhihirisha kwa ndugu zake.

Ndugu waliitikiaje pale Yusufu alipojidhihirisha kwao?

Ndugu hawakuweza kumjibu Yusufu kwa maana walikuwa wameshtushwa.

Genesis 45:7

Kulingana na Yusufu, kwa nini Mungu alimtuma Yusufu Misri?

Mungu alimtuma Yusufu Misri kuhifadhi uhai, na kutunza familia yake kama msalia wa duniani.

Mungu alimfanya Yusufu nini katika nchi ya Misri?

Mungu alimfanya Yusufu baba kwa Farao, bwana wa nyumba yote ya Farao, na mtawala juu ya nchi yote ya Misri.

Genesis 45:9

Yusufu alipangaje kuitunza familia yake?

Yusufu aliambia familia yake kuja na kuishi katika nchi ya Gosheni ambapo angewapa mahitaji.

Genesis 45:12

Yusufu aliwaambia ndugu zake kuharakisha kufanya nini?

Yusufu aliwaambia ndugu zake kuharakisha na kumleta baba yake Misri.

Genesis 45:16

Farao aliitikiaje aliposikia ya kwamba ndugu zake Yusufu wamekuja Misri?

Farao alipendezwa sana, na akamwambia Yusufu kuwaambia ndugu zake kumleta baba yao na nyumba zao kuishi katika nchi nzuri ya Misri.

Genesis 45:21

Ni nani alipokea zawadi za ziada na mgawanyo kwa ajili ya safari?

Benyamini alipokea vipande mia tatu vya fedha na mavazi matano ya kubadilisha, na Israeli alipokea punda ishirini ya punda waliobeba bidhaa.

Genesis 45:24

Israeli aliitikiaje aliposikia ya kuwa Yusufu alikuwa hai na mtawala wa nchi yote ya Misri?

Moyo wa Israeli ulishikwa na mshangao, kwa maana hakuamini ndugu walipomwambia.

Genesis 45:27

Israeli alisema alitaka kufanya nini kabla hajafa?

Israeli alisema alitaka kumuona Yusufu kabla hajafa.