Genesis 44

Genesis 44:1

Yusufu alimwambia mtunzaji wake wa nyumba kufanya nini na magunia ya ndugu zake kabla hawajaondoka?

Yusufu alimwambia mtunzaji wake wa nyumba kujaza magunia ya ndugu zake na chakula, na kuweka pesa yao ndani ya magunia, na kuweka kikombe chake cha fedha katika gunia la mdogo.

Genesis 44:3

Kwa hali ya kawaida Yusufu alimwambia mtunzanji wa nyumba kusema nini kwa ndugu alipowapita nje ya mji?

Yusufu alimwambia mtunzaji wa nyumba kuwauliza kwa nini walirudisha uovu kwa wema na kuwashtaki kuiba kikombe cha Yusufu.

Genesis 44:8

Ndugu waliapa wangefanya nini iwapo mmoja wao aliiba kikombe cha Yusufu?

Ndugu walisema mtu atakayekutwa na kikombe afe, na wengine wawe watumwa.

Adhabu gani mtunzaji wa nyumba alisema ilikuwa iwapo kikombe kiliibiwa?

mtunzaji wa nyumba alisema ya kwamba yule ambaye kikombe kitakutwa naye atakuwa mtumwa wake, na wengine watakuwa hawana hatia.

Genesis 44:11

mtunzaji wa nyumba alipata nini, na ndugu walichukuliaje?

mtunzaji wa nyumba alikuta kikombe katika gunia la Benyamini na ndugu zake wakararua nguo zao.

Genesis 44:14

Ndugu walifanya nini waliporudi katika nyumba ya Yusufu?

Ndugu waliinama chini mbele ya Yusufu hadi chini.

Genesis 44:16

Yuda alisema ni nani amegundua dhambi ya ndugu?

Yuda alisema ya kwamba Mungu aligundua dhambi yao.

Yuda alisema ndugu sasa watakuwa kina nani?

Yuda alisema ndugu wote sasa watakuwa watumwa wa Yusufu.

Yusufu alisema atahitaji adhabu gani kutoka kwa ndugu?

Yusufu alisema ya kwamba mtu ambaye mkono ulikuwa na kikombe atakuwa mtumwa wake, na wengine wangeondoka kwa amani.

Genesis 44:20

Yuda alitoa sababu zipi kwa nini baba yake alimpenda ndugu yao mdogo?

Yuda alisema ya kwamba ndugu yao mdogo alikuwa mtoto wa baba yake wa uzeeni, na mtoto pekee aliyebaki kwa mama yake.

Ndugu walikuwa na wasiwasi nini kingetokea kwa baba yao iwapo mdogo wao angemuacha?

Ndugu walikuwa na mashaka baba yao angekufa kama mdogo wao angemuacha.

Genesis 44:23

Yuda alisema ni kwa nini walilazimika kumleta Benyamini pamoja nao Misri?

Yuda alisema walilazimika kumleta Benyamini kwa sababu Yusufu alisema hadi pale ndugu yao mdogo aje, wasingeuona uso wa Yusufu.

Genesis 44:27

Israeli alidhani ni nini kilitokea kwa Yusufu?

Israeli alidhani ya kuwa hakika Yusufu aliraruliwa katika vipande.

Israeli alisema nini kingetokea kwake iwapo Benyamini angechukuliwa kutoka kwake?

Israeli alisema ya kwa ndugu wangeletea mvi kwa majonzi hadi kaburini.

Genesis 44:30

Yuda alisema nini kingetokea kwa baba yake iwapo watarudi bila Benyamini?

Yuda alisema ya kwamba baba yake angekufa.

Yuda alisema amekuwa uhakika gani kwa Benyamini?

Yuda alisema ya kwamba kama hatamrudisha Benyamini kwa baba yake, atabeba hatia milele.

Genesis 44:33

Yuda alimuuliza nini Yusufu kufanya ili kwamba Benyamini arudi kwa baba yake?

Yuda alimwomba Yusufu kumfanya awe mtumwa wa Yusufu, ili kwamba Benyamini aweze kurudi kwa baba yake.