Genesis 35

Genesis 35:1

Mungu alimwambia Yakobo kwenda wapi na kufanya nini?

Mungu alimwambia yakobo kwenda Betheli na kujenga madhabahu kwa Mungu.

Yakobo kisha aliwaambia watu wa nyumba yake kufanya nini?

Yakobo aliwaambia kuweka mbali miungu yao ya kigeni, na kujitakasa wenyewe, na kubadili mavazi yao.

Genesis 35:4

Kwa nini watu wa miji iliyozumzunguka Yakobo na nyumba yake hawakumfuata walipokuwa wakisafiri?

Watu wa miji iliyomzunguka hawakumfuata kwa sababu walimuogopa Mungu.

Genesis 35:6

Kwa nini Yakobo alipaita mahali walipofikia "El Betheli"?

Yakobo alipaita "El Betheli" kwa sababu ilikuwa mahali Mungu alijifunua kwa Yakobo pale Yakobo alipokuwa akimtoroka Esau.

Genesis 35:9

Mungu alimpatia Yakobo jina gani jipya?

Mungu alimpatia Yakobo jina jipya la Israeli.

Genesis 35:11

Mungu alithibitisha ahadi gani kwa Yakobo?

Mungu alithibitisha ahadi ya kwamba Yakobo atakuwa kundi la mataifa lenye wafalme miongoni mwa uzao wake, na kwamba nchi ambayo Mungu alimuahidi Abrahamu na Isaka itapewa kwake na uzao wake.

Genesis 35:16

Nini kilitokea kwa Raheli wakati wa uchungu wake kwa Benyamini?

Raheli alikufa wakati wa uchungu kwa Benyamini.

Genesis 35:21

Israeli alisikia kuhusu jambo gani ambalo Rubeni alifanya?

Israeli alisikia ya kwamba Rubeni alilala na Bilha, suria wa Israeli.

Yakobo alikuwa na wana wangapi wa kiume?

Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili.

Genesis 35:23

Watoto gani wa Yakobo walizaliwa kutoka kwa Raheli

Yusufu na Benyamini walizaliwa kutoka kwa Raheli.

Genesis 35:28

Isaka aliishi miaka mingapi?

Isaka aliishi miaka mia moja na themanini.

Nani alimzika Isaka?

Esau na Yakobo walimzika Isaka.