Genesis 31

Genesis 31:1

Labani na wanawe waliamini Yakobo alipata wapi utajiri wake wote?

Labani na wanawe waliamini ya kwamba Yakobo alipata utajiri wake kutoka kwa mali za Labani.

Yahwe alitoa maelekezo yapi kwa Yakobo?

Yahwe alimuelekeza Yakobo kurudi katika nchi ya baba zake na ndugu zake.

Genesis 31:7

Mungu alichukuaje mifugo wa Labani na kumpatia Yakobo?

Mungu alisababisha wanyama kuwa na mabaka, na watoto wao kuwa na milia ambayo ilikuwa ujira wa Yakobo.

Genesis 31:14

Raheli na Lea walikuwa na mtazamo gani dhidi ya baba yao Labani?

Raheli na Lea walisema ya kwamba Labani aliwatendea kama wageni na alitapanya pesa yao.

Genesis 31:19

Raheli alifanya nini kabla ya kuondoka na Yakobo?

Raheli aliiba miungu nyumbani mwa baba yake.

Yakobo alimdanganyaje Labani katika kipindi hiki?

Yakobo alimdanganya Labani kwa kutomuambia ya kuwa alikuwa akiondoka.

Genesis 31:22

Labani alifanya nini alipoambiwa ya kuwa Yakobo ametoroka?

Labani alichukua ndugu zake pamoja naye na kumfuata Yakobo, na kumpita baada ya siku saba.

Genesis 31:24

Mungu alimwambia nini Labani katika ndoto?

Mungu alimwambia Labani kutozungumza jambo jema au baya kwa Yakobo.

Genesis 31:31

Yakobo alisema ni kwa nini alimtokoka Labani kwa siri?

Yakobo alisema ametoroka kwa siri kwa sababu aliogopa ya kwamba Labani angewachukua binti zake kutoka kwake kwa nguvu.

Yakobo alisema nini pale Labani alipomtuhumu kuiba miungu ya nyumba yake?

Yakobo alisema ya kwamba yeyote aliyeiba miungu ya nyumba ya Labani hataendelea kuishi.

Genesis 31:34

Kwa nini Labani hakuipata miungu ya nyumba yake miongoni mwa mali za Yakobo?

Labani hakuipata miungu ya nyumba yake kwa sababu Raheli alikuwa amekalia na kisha akasema ya kwamba hakuweza kusimama kwa kuwa alikuwa katika kipindi cha hedhi.

Genesis 31:41

Yakobo alifanya kazi miaka mingapi kwa Labani, na mara ngapi Labani alibadili ujira wake?

Yakobo alifanya kazi kwa Labani miaka ishirini, na Labani alibadili ujira wake mara kumi.

Genesis 31:43

Labani alionyeshaje ya kuwa alidhania utajiri wa Yakobo bado ni wa kwake?

Labani alisema ya kwamba kila alikiona ni mali ya Yakobo kilikuwa chake.

Genesis 31:45

Yakobo na Labani waliweka alama gani katika nafasi ya agano lao?

Yakobo na Labani waliweka alama mahali pale pa agano kwa kupanga rundo la mawe.

Genesis 31:48

Ni nani alitajwa kuwa shahidi kati ya Yakobo na Labani kuhakikisha agano litatunzwa?

Mungu alitajwa kuwa shahidi kati ya Yakobo na Labani kuhakikisha agano litatunzwa.

Genesis 31:51

Rundo na nguzo zilikuwa kwa ajili ya nini?

Rundo na nguzo zote zilikuwa mashahidi kwa ajili ya agano ambalo lilisema ya kuwa Labani wala Yakobo hawatapita rundo au nguzo ile kwa kumdhuru mwenzake.

Ni agano gani Yakobo na Labani walifanya?

Yakobo na Labani kila mmoja alikubaliana kutopita ng'ambo ya pili ya rundo na mawe kumdhuru mwenzake.

Yakobo alifanya nini kuonyesha alikubaliana na agano jilo?

Kuonyesha ya kuwa alikubaliana na Labani juu ya agano Yakobo aliapa kwa Mungu, ambaye baba yake Isaka alimcha.

Genesis 31:54

Labani alifanya nini asubuhi iliyofuata?

Labani aliamka, akawabusu wajukuu na mabinti zake, akawabariki, na kurudu nyumbani.