Genesis 30

Genesis 30:1

Kulingana na Yakobo, kwa nini Raheli hakuwa na watoto?

Kulingana na Yakobo, Mungu alimzuia Raheli kupata watoto.

Genesis 30:3

Raheli alifanya nini ili apate watoto?

Raheli alimpatia Bilha kwa Yakobo mtumishi wake ili aweze kupata watoto kwa niaba ya Raheli.

Genesis 30:7

Kwa nini Raheli alisema alishinda dhidi ya dada yake Lea?

Raheli alisema ya kwamba alishinda kwa sababu Bilha mtumishi wake alimzalia watoto wawili kwa Yakobo.

Genesis 30:9

Lea alifanya nini alipoona ya kwamba ameshindwa kupata watoto?

Lea alimpatia Yakobo mtumishi wake Zilpa ili aweze kupata watoto kwa niaba ya Lea.

Nini kilisababisha Lea kusema, "Hii ni bahati njema!"

Lea alisema, "Hii ni bahati njema" kwa sababu Zilpa mtumishi wake alimzalia Yakobo mtoto wa kiume.

Genesis 30:14

Raheli alitoa nini kwa Lea ili kubalishana kwa tunguja za mwanawe?

Kwa kubadilishana na tunguja za Rubeni, Raheli alitoa kumruhusu Lea alale na Yakobo usiku huo.

Genesis 30:19

Lea alimzalia Yakobo wana wa kiume wangapi?

Lea alizaa wana wa kiume sita kwa Yakobo.

Genesis 30:22

Nini kilisababisha Raheli kusema ya kwamba aibu yake imetoweka?

Raheli alipomzaa mwana kwa Yakobo, alisema ya kwamba aibu yake imeondoka.

Genesis 30:25

Yakobo alitoa ombi gani kwa Labani baada ya Yusufu kuzaliwa?

Yakobo aliomba ya kwamba Labani amruhusu Yakobo aondoke na familia yake na kurudi kwa nyumba na nchi yake.

Genesis 30:27

Kwa nini Labani hakutaka Yakobo aondoke?

Labani aligundua ya kwamba Mungu alimbariki yeye kwa niaba ya Yakobo.

Genesis 30:31

Yakobo alipokea ujira upi kwa kazi kwa ajili ya Labani?

Yakobo alichukua kondoo wenye milia, mabaka na weusi na mbuzi wenye milia na mabaka kutoka kwa kundi la Labani aliowachunga.

Genesis 30:35

Labani alimdanganyaje Yakobo kuhusu ujira wa Yakobo?

Labani aliwatoa kwanza wanayma ambao Yakobo angewachukua, kabla hajawapa kwa Yakobo kuwachunga.

Genesis 30:37

Yakobo alitoa maganda ya matawi gani yenye mchirizi myeupe?

Yakobo alitoa maganda yenye michirizi myeupe katika matawi ya mipopla, mlozi na mwaroni mbichi.

Yakobo alifanya nini na fito alizokuwa amezibambua?

Yakobo akaziweka fito alizokuwa amezibambua mbele ya makundi ya kondoo, mbele ya mabirika yakunyweshea walipokuja kunywa maji.

Genesis 30:39

Nini kilitokea wanyama walipopanda mbele ya fito?

Wanyama wakapandana mbele ya fito; nao wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa

Genesis 30:41

Nini ilikuwa matokeo ya upandaji wa Yakobo wa wanyama?

Matokeo yake yakawa kwamba wanyama wa Labani wakawa dhaifu, na wanyama wa Yakobo wakawa wenye nguvu.