Genesis 28

Genesis 28:1

Isaka alitoa amri gani kwa Yakobo kabla hajaondoka?

Isaka alimuamuru Yakobo kutochukua mke wa Kaanani.

Isaka alimwambia Yakobo kuchukua mke mahali gani?

Isaka alimwambia kuchukua mke kutoka kwa mabinti wa Labani, kaka wa Rebeka.

Genesis 28:3

Ni baraka ya nani ambayo Isaka alimuomba Mungu ampatie Yakobo?

Isaka alimwomba Mungu ampatie Yakobo baraka ya Abrahamu.

Genesis 28:8

Esau alipata mmoja wa wake zake kutoka wapi alipogundua ya kwamba wanawake wa Kaanani hawakumpendeza Isaka?

Esau alichukua mke kutoka kwa binti wa Ishmaeli, mwana wa Abrahamu.

Genesis 28:12

Yakobo aliona nini katika ndoto alipokuwa njiana kwenda Harani?

Yakobo aliona ngazi kutoka kwenye nchi kwenda mbinguni na malaika wakipanda na kushuka juu yake, na Yahwe akisimama juu yake.

Yahwe alisema nini kuhusu nchi ambayo Yakobo aliyokuwa amelala juu yake?

Yahwe alisema ya kwamba nchi ambayo Yakobo amelala juu yake itapewa kwake na kwa uzao wake.

Ni baraka ya nani Yahwe alimpatia Yakobo?

Yahwe alimpatia Yakobo baraka ya Abrahamu.

Genesis 28:16

Yakobo alisema nini kuhusu mahali ambapo alipata ndoto ile?

Yakobo alisema mahali pale palikuwa nyumba ya Mungu na lango la mbinguni.

Genesis 28:18

Ni jina gani alilolipa Yakobo mahali pale ambapo alipata ile ndoto?

Yakobo alipaita mahali pale Betheli.

Genesis 28:20

Yakobo alisema Yahwe anapaswa kufanya nini ili kwamba Yahwe aweze kuwa Mungu wake?

Yakobo alisema ya kwamba Yahwe anapaswa kuwa pamoja naye na kumlinda katika safari yake ili kwamba arudi salama kwa nyumba ya baba yake.

Yakobo aliahidi kumpataia nini Yahwe iwapo Yahwe angefanya mambo haya kwake?

Yakobo aliahidi kumrudishia Yahwe moja ya kumi ya kila kitu Yahwe alichompatia Yakobo.