Genesis 17

Genesis 17:1

Abramu alikuwa na umri gani Yahwe alipomtokea tena kuthibitisha agano lake pamoja naye?

Abramu alikuwa na miaka tisini na tisa Yahwe alipomtokea tane Abramu.

Yawhe alimpatia Abramu amri gani kuhusu njia ya maisha ya Abramu?

Yahwe alimuamuru Abramu kuenenda mbele yake kikamilifu.

Genesis 17:3

Yahwe alibadili jina la Abramu kuwa nani, na jina lina maana gani?

Yahwe alibadili jina la Abramu kuwa Abrahamu ambayo ina maana ya "baba wa mataifa mengi"

Genesis 17:7

Yahwe alitoa nini kwa vizazi vya Abrahamu kama sehemu ya agano?

Yahwe aliwapa vizazi vya Abrahamu nchi yote ya Kaanani kama sehemu ya agano.

Yahwe alisema mahusiano kati ya vizazi vya Abrahamu na Yahwe yangekuwaje?

Yahwe alisema ya kwamba angekuwa Mungu kwa vizazi vya Abrahamu.

Genesis 17:9

Yahwe aliamuru nini kifanyike kama ishara ya agano kati ya Abrahamu na Yahwe?

Yahwe aliamuru ya kwamba kila mwanamume altahiriwe kama ishara ya agano kati ya Abrahamu na Yahwe.

Genesis 17:12

Mtoto alitahiriwa katika umri gani?

Mtoto alipaswa kutahiriwa baadaya siku nane.

Mgeni aliyejiunga na familia ambayo ilikuwa na agano na Yahwe ilipaswa kufanywa nini?

Wageni waliojiunga na nyumba iliyokuwa ndani ya agano na Yahwe pia walipaswa kutahiriwa.

Nini kilitokea kwa mwanamume yeyote ambaye hakutahiriwa?

Mwanamume yeyote ambaye hakutahiriwa alitengwa na watu wake kwa sababu alivunja agano.

Genesis 17:15

Yahwe alibadili jina la Sarai kuwa nani?

Yahwe alibadili jina la Sarai kuwa Sara.

Yahwe aliahidi kungekuja nini kwa Sara?

Yahwe aliahidi ya kwamba mwana wa Abrahamu angekuja kwa Sara.

Genesis 17:17

Ni kwa namna gani Abrahamu alichukulia ahadi ya Yahwe kuhusu Sara?

Abrahamu alicheka na kuuliza ni namna gani mtoto anaweza kuzaliwa kwa mwanamume na mwanamke ambao ni wazee sana.

Genesis 17:19

Mungu alisema Abrahamu alipaswa kumpatia jina lipi mwanawe ambaye angekuja kwa Sara?

Mungu alisema ya kwamba Abrahamu anapaswa kumtaja mwanawe Isaka.

Mungu alisema angethibitisha nini na Isaka?

Mungu alisema ya kwamba angethibitisha agano lake na Isaka.

Mungu alitoa ahadi gani kuhusu Ishmaeli?

Mungu aliahidi kumbariki Ishmaeli, kumzidishia, na kumfanya kuwa taifa kubwa.

Genesis 17:24

Abrahamu alifanya nini katika siku hiyo, baada ya Mungu kumuacha Abrahamu?

Katika siku hiyo, Abrahamu alitahiri wanamume wote wa nyumba yake.

Ishmaeli alikuwa na umri wa miaka mingapi alipotahiriwa?

Ishmaeli alikuwa na umri wa miaka kumi na tatu alipotahiriwa.