Genesis 16

Genesis 16:1

Sarai alikuwa na wazo gani kwa ajili ya kumpatia Abramu uzao?

Sarai alimwambia Abramu kulala na mtumishi wake Hajiri, ili kwamba apate watoto kupitia kwake.

Nini kilitokea kati ya Hajiri na Sarai pale Hajiri alipobeba mimba ya mtoto wa Abramu?

Baada ya Hajiri kushika mimba, Hajiri alimdharau Sarai.

Genesis 16:5

Sarai alitoa malalamiko gani kwa Abramu, na Abramu aliitikiaje?

Sarai alilalamika ya kwamba lilikuwa kosa la Abramu kwa Hajiri kumdharau, na Abramu akamwambia Sarai kufanya alichofikiri ni sahihi kwa Hajiri.

Sarai alimtendeaje Hajiri baada ya Hajiri kupata mimba, na Hajiri alifanyaje?

Sarai alimtendea ukatili Hajiri, na Hajiri alitoroka.

Genesis 16:9

Malaika wa Yahwe alimwambia Hajiri kufanya nini katika jangwa?

Malaika wa Yahwe alimwambia Hajiri kurudi kwa Sarai na kujishusha chini ya mamlaka yake.

Malaika wa Yahwe alitoa ahadi gani kwa Hajiri?

Malaika wa Yahwe alimuahidi Hajiri ya kwamba vizazi wake watakuwa wengi wasioweza kuhesabika.

Genesis 16:11

Kwa nini Hajiri aliambiwa kumuita mwanawe Ishmaeli?

Hajiri aliambiwa kumuita mwanawe Ishmaeli kwa sababu Yahwe amesikia mateso yake.

Ishmaeli atawatendeaje watu wengine?

Ishmaeli atakuwa na uhasama dhidi ya kila mtu, na ataishi kando na ndugu zake wote.

Genesis 16:13

Hajiri alimpatia jina gani Yahwe?

Hajiri alimpatia Yahwe jina la, "Mungu anayeniona"

Genesis 16:15

Abramu alikuwa na umri gani Ishmaeli alipozaliwa?

Abramu alikuwa na umri wa miaka themanini na sita Ishmaeli alipozaliwa.