Genesis 9

Genesis 9:1

Mungu alimwambia nini Nuhu na wanawe kufanya baada ya kutoka katika safina?

Mungu alimwambia Nuhu na wanawe kuzaana, kuongezeka na kujaza nchi.

Genesis 9:3

Mungu alimpatia nini Nuhu na wanawe sasa kama chakula?

Mungu alimpatia Nuhu na wanawe wote mimea ya kijani na kila kitu chenye uhai kama chakula.

Mungu aliamuruje ile nyama iweze kuliwa kwa namna gani?

Mungu aliamuru ya kwamba nyama isiliwe na damu ndani mwake.

Mungu alisema ni nini kimo ndani ya damu?

Mungu alisema ya kwamba kulikuwa na uhai ndani ya damu.

Genesis 9:5

Mungu alitamka ni adhabu gani kwa kumwaga damu ya binadamu?

Mungu alitamka ya kwamba yule atakayemwaga damu ya mtu atalazimika kumwaga damu yake.

Mungu alimfanya mwanadamu kwa mfano wa nani?

Mungu alimfanya mwanamume katika mfano wa Mungu.

Genesis 9:11

Mungu alitoa ishara gani kama agano alilofanya pamoja na nchi?

Mungu aliweka upinde wa mvua katika mawingu kama ishara ya agano alilofanya pamoja na nchi.

Genesis 9:14

Mungu alifanya ahadi gani ya agano na kila kitu kilichokuwa kikiishi juu ya nchi?

Mungu alifanya agano la ahadi ya kwamba kila chenye mwili hatakiangamiza kwa gharika tena.

Genesis 9:18

Majina ya wana wa Nuhu yalikuwa ni yapi?

Majina ya wana watatu wa Nuhu yalikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi.

Genesis 9:20

Nini kilitokea kwa Nuhu baada ya kupanda mizabibu?

Baada ya kupanda mizabibu, Nuhu alikunywa sehemu ya divai na akalewa.

Genesis 9:22

Shemu na Yafethi walifunikaje uchi wa baba yao?

Shemu na Yafethi walitembea kinyumenyume na kanzu, huku wakiwa wametazama upande mwingine, ili kufunika uchi wa baba yao.

Genesis 9:24

Nuhu aliweka laana gani juu ya Hamu?

Nuhu alimlaani Hamu na kusema, "Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake"

Genesis 9:26

Nuhu alimbariki nani?

Nuhu aliwabariki wote Shemu na Yafethi.