Genesis 8

Genesis 8:1

Mungu alifanyaje maji kupungua?

Mungu alifanya upepo kuvuma, chemichemi za vilindi kufungwa, na mvua kusimama.

Genesis 8:4

Safina lilikuja kutulia wapi juu ya nchi?

Safina lilikuja kutulia juu ya milima ya Ararati.

Genesis 8:8

Nini kilitokea mara ya kwanza Nuhu alipomtuma njiwa kutoka kwenye safina?

Mara ya kwanza, njiwa hakupata sehemu ya kutua nyayo zake, na akarudi kwa Nuhu katika safina.

Genesis 8:10

Nini kilitokea mara ya pili Nuhu alipomtuma njiwa kutoka katika safina?

Mara ya pili, njiwa alirudi na jani bichi la mzeituni lililochumwa.

Nini kilitokea mara ya tatu Nuhu alipomtuma njiwa kutoka katika safina?

Mara ya tatu, njiwa hakurudi kwa Nuhu.

Genesis 8:13

Nuhu aliona nini alipotoa kifuniko cha safina na kutazama nje?

Nuhu aliona ya kwamba uso wa nchi ulikuwa umekauka.

Genesis 8:15

Mungu alitaka viumbe wote katika safina kwenda kufanya nini walipotoka katika safina?

Mungu alitaka viumbe wote hai kuzaana na kuongezeka juu ya nchi.

Genesis 8:20

Nuhu alifanya nini alipoondoka katika safina?

Nuhu alijenga madhabahu kwa ajili ya Yahwe na sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu.

Ahadi gani mbili Mungu alizifanya kwa wanadamu katika kipindi hiki?

Mungu aliahidi kutolaani tena ardhi, na kutoangamiza kila kiumbe hai tena.

Mungu alisema mwanadamu ana nia gani tangu utoto wake?

Mungu alisema ya kwamba nia ya mwanadamu kutoka utotoni ilikuwa ni ya uovu.