Genesis 2

Genesis 2:1

mbingu

"anga" au "mbingu"

na viumbe hai vyote vilivyo jaza

"na viumbe hai vingi ambavyo vimo ndani yao" au "na makundi ya viumbe hai vinavyoishi ndani mwao"

zilimalizika

Hii inaweza kutajwa katika njia endelevu "Mungu alimaliza kuviumba"

Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake

Mungu hakufanya kazi kabisa katika siku ya saba.

alifikia mwisho wa

Hii ni lahaja. "alikuwa amemaliza"

alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote

"katika siku hiyo hakufanya kazi"

Mungu akaibarikia siku ya saba

Yawezekana maana ni 1) Mungu alisababisha siku ya saba kutoa matokeo mazuri au 2) Mungu alisema ya kwamba siku ya saba ilikuwa nzuri.

na akaitakasa

"na akaiweka kando" au "na kuifanya iwe yake"

katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote

"katika siku hiyo hakufanya kazi"

Genesis 2:4

Taarifa ya jumla

Sura ya pili iliyobaki ya Mwanzo inaelezea juu ya Mungu alivyoumba watu katika siku ya sita.

Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi

"Hii ni habari ya mbingu na nchi" au "Hii ni simulizi ya mbingu na nchi" Yawezekana maana ni 1) ni kifupisho cha matukio yaliyoelezwa katika Mwanzo 1:1-2:3 au 2) inakaribisha matukio yaliyoelezwa katika Mwanzo 2.

vilipoumbwa

Yahwe Mungu aliviumba". Katika sura ya 1 mwandishi kila mara anamzungumzia Mungu kama "Mungu", lakini katika sura ya 2 kila mara anamzungumzia Mungu kama "Yahwe Mungu".

katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba

"Yahwe Mungu alipoumba". neno "siku" linamaana ya muda wote wa uumbaji na siyo siku hiyo moja pekee.

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Hapakuwa na msitu wa shambani

hapakuwa na vichaka vimeavyo msituni ambayo wanyama wangeweza kula

hapakuwa na mmea wa shambani

hapakuwa na mimea ya majani kama mboga au mboga za kijani ambazo wanyama na binadamu wangeweza kula

kulima

kufanya kila kitu alichopaswa kufanya ili kwamba mimea iweze kuota vizuri

ukungu

Yawezekana maana yake ni 1) kitu kama umande au ukungu wa asubuhi au 2) chemichemi kutoka mikondo chini ya ardhi.

uso wote wa ardhi

dunia nzima

Genesis 2:7

aliumba

"alifinyanga" au "alifanya" au "aliumba"

mtu ... mtu

"binadanu ... mtu" au "mwanadamu" sio lazima wa kiume.

tundu la pua

"pua yake"

pumzi ya uhai

"pumzi inayofanya vitu kuishi". Hapa "uhai" una maana ya uhai wa mwili.

bustani

Hii yaweza kuwa shamba la miti ya matunda au eneo lenye kila aina ya miti.

upande wa mashariki

"mashariki"

Genesis 2:9

mti wa uzima

"mti unaowapa watu uzima"

uzima

Hapa ina maana "uzima wa milele" au maisha yasiyokuwa na mwisho.

mti wa ujuzi wa mema na mabaya

"mti unaowapa watu uwezo wa kuelewa mema na mabaya" au "mti unaowafanya watu wale matunda yake na kuwafanya kuelewa mema na mabaya"

mema na mabaya

Huu ni msemo ambao una maana mbili tofauti kabisa na kila kitu katikati. "kila kitu kujumlisha yote mema na mabaya"

katikati ya bustani

"katikati ya bustani". Yawezekana miti hii miwili haikuwa katikati ya bustani kabisa.

Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani

Bustani ilikuwa Edeni. Mto uliendelea kutiririka kutoka Edeni. "Mto ukatoka kupitia Edeni na kumwagilia bustani"

Genesis 2:11

Pishoni

Huu ni wakati pekee ambapo mto huu unatajwa katika Biblia.

nchi yote ya Havila

"nchi yote inaitwa Havila". Ilikuwa mahali katika jangwa la Arabia.

ambapo kuna dhahabu

Msemo huu unatoa taarifa kuhusu Havila. Baadhi ya lugha hutafsiri kwa sentensi nyingine tofauti. "Kuna dhahabu Havila"

pia kuna bedola na jiwe shohamu

Neno "kuna" lipo kwenye sentensi kwa kuonyesha msisitizo. "Hapa pia ni mahali ambapo watu waweza kupata bedola na mawe ya shohamu"

bedola

Utomvu huu hutoka katika mti na hutoa harufu nzuri. Bedola hunata na hutoka katika mti fulani na yaweza kuwaka moto.

jiwe shohamu

"mawe ya shohamu". Shohamu ni aina fulani ya mawe ya urembo.

Genesis 2:13

Gihoni

Hii ni sehemu pekee ya mto huu katika Biblia.

unatiririka kupitia nchi yote ya Kushi

Mto haukufunika nchi yote, lakini ulipanda katika sehemu za nchi.

nchi yote ya Kushi

"nchi nzima inayoitwa Kushi"

ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru

"ambao unatiririka katika nchi mashariki mwa mji wa Ashuru." Mto wa Hidekeli unatiririka kutoka kaskazini hadi kusini. Msemo "unatiririka mashariki mwa Ashuru" unatoa taarifa kuhusu mahali mto Hidekeli ulipo. Baadhi ya lugha hutafsiri katika sentensi tofauti. "na hutiririka mashariki mwa Ashuru"

Genesis 2:15

bustani ya Edeni

"bustani iliyokuwa Edeni"

kuilima

"kuilima". Hii ina maana ya kufanya kila kitu cha muhimu ili mimea iweze kuota vizuri.

kuitunza

kuilinda dhidi ya mambo mabaya yanayoweza kuikuta

kutoka kwenye kila mti bustanini

"Tunda katika kila mti la bustani"

wewe

kiwakilishi ni cha kipekee

waweza kula kwa uhuru ...usile

Katika baadhi ya lugha ni kawaida kusema kile ambacho hakiruhusiwi na kisha kusema kile ambacho hakiruhusiwi.

waweza kula kwa uhuru

"waweza kula bila kizuizi"

mti wa ujuzi wa mema na mabaya

"mti unaowapa watu uwezo wa kuelewa mema na mabaya" au "mti unaowafanya watu wanaokula matunda yake kujua mambo mazuri na mambo mabaya.

usile

"sitakuruhusu ule" au "haupaswi kula"

Genesis 2:18

Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa

"nitafanya msaidizi ambaye ni sahihi kwa ajili yake"

kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani

Misemo ya "wa kondeni" na "wa angani" inatuambia mahali ambapo wanyama na ndege hupatikana mara kwa mara. "kila aina ya wanyama na ndege"

wanyama wote

"wanyama wote ambao watu huwachunga"

hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hapakuwa na msaidizi aliyekuwa sahihi kwa ajili yake"

Genesis 2:21

akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu

"alisababisha mwanamume kulala sana." Usingizi mzito ni wakati ambapo mtu kalala na hawezi kubughudhiwa kirahisi au kuamshwa.

Kwa ubavu ... akafanya mwanamke

"Kutoka ubavuni... alimuumba mwanamke." Ubavu ni nyenzo ambayo Mungu alimuumba mwanamke.

kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu

"Hatimaye, mifupa ya huyu ni kama ya kwangu, na nyama yake ni kama nyama yangu". Baada ya kutazama miongoni mwa wanyama wote kwa ajili ya mwenzi na kukoswa, hatimaye akamwona mtu kama yeye ambaye angeweza kuwa mwenzi wake. Yawezekana mwanamume alionyesha hisia za faraja na furaha.

nyama

Hii inamaanisha sehemu laini za mwili kama ngozi na msuri.

ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume

"Neno la Kihebrania la 'mwanamke' linafanana na neno la Kihebrania kwa ajili ya 'mwanamume'.

Genesis 2:24

Taarifa ya jumla

Kinachofuata kimeandikwa na mwandishi. Mwanamume hakusema vitu hivi.

Kwa hiyo

"Hii ni kwa sababu"

mwanaume atawaacha baba yake na mama yake

"mwanamume ataacha kuishi kwenye nyumba ya baba na mama yake." Hii inahusu wanamume kwa ujumla. Hailengi mwanamume fulani katika muda fulani.

watakuwa mwili mmoja

Lugha hii inaongelea tendo la ngono kana kwamba miili inakutana pamoja na kuwa kama mwili mmoja. "miili yao miwili itakuwa mwili mmoja"

Wote wawili walikuwa uchi

Neno "walikuwa" linamaana ya mwanamume na mwanamke ambao Mungu aliwaumba.

uchi

"kutovaa mavazi"

lakini hawakuona aibu

"hawakuona aibu kwa kuwa uchi"