Sula 2

1 Mu tupe seke bubaya bote na bukalamishi bote , bunafiki, tama, na bunafiki bote , 2 Mutake , sa vile batoto bana zarika sasa , maziwa ya kiroho na kutakasiwa, djo kupitiya yeye mwendeleye dju ya ku okolewa, 3 Kama muri pima Bwana eko muzuri. 4 Mu tshofe karibu na ye , Ribwe ria bujima , ile bantu bari tupa , Lakini iri tshakuliwa na kufuraiwa kumbele ya Mungu; 5 Na mwebenyyewe , sa maibwe ya bujima , murifundishe dju ya kuya nyumba ya kiroho , kaji takatifu, djo ya ku towa ya kiroho, ya kupendeza Mungu kupitiya Yesu-Kristo. 6 Kwamana Mwandjiko ina sema : Ona , mina weka mu Siona Ribbwe ya ushimamo , ile iri tshakuliwa , ya lazima ; Na ule ana aminiya mwake ashi takuya na aya. 7 Echima iko seke dju yenu , muna aminiya. Lakini , dju ya basho kwamini , ribwe ile bana tupa kwa bale barianza ku yenga ina kuya Ushimamo, 8 Na ribwe ya kuterezika na ribwe rinene ya muvuroko, beko na ribuntula dju aba echimiye wala ku amini neno , na ni kwa ile bari batayarishiya. 9 Mweye , muko bantu ba ku tshakuliwa , kikudji kia bafalme , mataifa ya batakatfu, bantu yake , djo ya sema buzuri ya ule ari mi ita kutoka ngiza paka mwanga yake ya furah, 10 mweye ku mashiku ya kumukongo amu kukuye bantu ba Mungu , na bale sasa munakuya bantu ba Mungu, mweye a mu kupate rehema , na sasa muna pata rehema. 11 Mupendua , mi na misubutisha , sa vile bageni na ba kupita apa ba dunia, mu kuye bari na furah ya kimwili ile iku na kombanisha nafsi . 12 Mu kuye na mifano muzuri, djo kama bana misema mu bubaya , ba one mifano yenu muzuri , na ba tukuze Mungu, shiku ile ata batembeleya. 13 Mukuye baku ti , djo ya Bwana , ku ba uongozi bote bari ba weka kwa bantu, wala Mufalme sa vile bakubwa, 14 wala ku ba tchungadji vile bari batuma kupitiya yeye dju ku nyolosha bale bana fanya mambo mubaya na dju ya ku onesha bantu bazuri. 15 Kwamana ni mapenzi ya Mungu muku fanya bizuri mu na epusha bantu ba bumbafu ba seme ile a ba djuwe, 16 Mukuya uru , pashipo ku fanya ile uru guwo ina funika bubaya , lakini mu ishi sa ba tumishi ya Mungu. 17 Mwe shimiye bantu bote ; mupendez ba nduku ; mongope Mungu ; mwe shimiya mufalme. 18 Batumishi , mukuye ba kurishusha kwa ba mwarimu yenu , ayina paka kwa bae beko bien na kimia , lakini tena kwa bale bko na mifano ya nguvu. 19 Kwalakini ni neema kuliko ku itshikiya mateso kupitiya matokewo ya samiri kwa Mungu ,kama tu na teswa mubaya bila aki . 20 Lakini , ni `utukufukani iko pale kwitshikiya kuteswa dju uri fanya ma kosa? Lakini kama muna itshikiya mateso pale muna fanya ile iko muzuri, ni neema bele ya Mungu. 21 Na Ni kwa ile bari mi itiya , djo Kristo tena ari teswa dju yenu , ana miatshiya mwenedo, djo mu fate ma djiya yake , 22 Yeye ashi ku fanye zambi, na mu kinya kile a mu kutoke bongo; 23 Yeye ule , bari mutshambula , ashi kwanze ku rudisha ma matushi ; ba na muteswa , ashi ku fanye fudjo , lakini ariangaria ule ana sambishaka na ukweli. 24 Yeye ari beba ye moya ma zambi mu mwili yake ku mu salaba , djo akufe mu zambi shiye tu ishi dju ya aki ; Yeye kupitiya bilonda biake bile muri pata matuzo . 25 Kwamana muri kuya sa vile ba kondo ba sha kwenda ku pepeni . Lakini sasa muna rudiya kwa mutshungadji na mutshungadji ya ma nafsi yenu.