Sura 1

1 Paulo mufungwa wa Kristo Yesu, pamoja na ndugu Timoteo, kwa Filemoni mwenzetu katika huduma. 2 Kwa data yetu Afiya, Archipu mupiganaji mwenzetu, na kwa kanisa muzima yenye inakusanyika ndani ya nyumba yako. 3 Neema na amani kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana Yesu Kristo bikuwe kwenu. 4 Minaendelea kushukuru Mungu wangu. Na mina kukumbukaka mu maombi yangu. 5 Nilipata habari kuhusu mapendo na imani yenye ukonayo ndani ya Bwna Yesu Kristo na kwa waamini wote. 6 Nina omba kusudi ushirika wa imani yako ukamilike kusudi ujue nini ya muhimu yenye iko kati yetu ndani ya Kristo. 7 Kwa sababu niko na furaha na mina farijika ju ya mapendo yako, ulifariji roho za baamini bote ndugu yangu. 8 Hivi, hata kama niko na jurudi ndani ya Kristo na ruhusa ya kukupa amuri ya kufanya kazi yako, 9 Lakini sababu ya mapendo mina kuomba (miye mzee Paulo mu fungwa ju ya Yesu). 10 Na ku sihi sababu ya mutoto yangu Onesime mwenye nili zala ndani ya mabusu. 11 Zamani alikua hana mafaa kwako. Lakini leo anakuwa na mafaa kwako na kwangu. 12 Nimekurudishia naye hata kama iko wamuhimu ndani ya roho yangu. 13 Ningependa abakiye na miye kusudi ani saidie ndani ya hii magumu ya kifungo, sababu ya habari njema. 14 Lakini sikupenda kuifanya, iliomba tukubaliane na weye. Sikupenda bizuri byenye utafanya bitokane na kusukumwa lakini itokane na kutaka kwako. 15 Ina wezekana alitengwa kwako kwa wakati kidogo kusudi akurudilie na abakie na weye siku yote. 16 Hatakuwa tena mutumwa, lakini kushinda mutumwa, yeye ni ndugu mpendwa, zaidi kwangu na kwako katika mwili na ndani ya Bwana. 17 Na kwa hiyo kama una nipokea kama mupendwa mupokee naye kama miye. 18 Kama aliku tendeaka mabaya, wala iko na deni yako, uniulize miye. 19 Mimi Paulo, minaandika hii kwa mukono yangu mi peke, nitakurudishia byote. Sikupenda kusema unipe maisha yako yote. 20 Ndugu yangu nakuomba sana katika Bwana Yesu Kristo upumuzishe roho ya ngu tafazali. 21 Kama mina kuandikia ni ju mina kutumainia, na jua kama utafanya zaidi ya ile minakuomba. 22 Pamoja na ile uni tayarishie chumba moya munyumba ya wageni, sababu mina tumainia kama kupitia maombi yenu nitabafikia. 23 Epafra, mwenzangu mufungwa katika Kristo Yesu, ana kusalimia, 24 Pia na Marko, Aristariki, Demasi, na Luka benzangu ba kazi. 25 Neema ya bwana Yesu Kristo ibaki ndani ya roho yako. Amen