Sura 1

1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu na Timeteo ndugu wetu. 2 Kwa waaminifu na wandugu katika Kristo. Neema na amani ya Mungu Baba ikue pamoya na nyiye. 3 Tunashukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na tunawaombea kila siku. 4 Tulisikia Kuhusu imani yenu katika Yesu kristo, na mapendo yenye muko nayo kwa wachaguliwa wa Mungu. 5 Muko na mapendo kwa sababu ya tumaini yenye inatayarishiwa kwa ajili yenu mbinguni,mulisikia wakisema juu ya ile tumaini katika neno la kweli, habari njema yenye iliwafikiya. 6 Habari njema hii ilizaa matunda na kuhubiriwa Duniani , Ilifanyika hivi kwenu pia tika siku muliyoisikiya na kujifunza kuhusu neema ya Mungu na kweli, 7 Hii habari njema kama mulivyo isikiya kwa Epafra mtumishi mwenzetu na mpendwa , mwaaminifu na mtumishi wa Kristo kwa ajili yet . 8 Epafra alitujulisha kuhusu mapendo yenu katika Roho. 9 Hatukuacha kumiombeya toka siku tulisikia kuhusu upendo wenu, Tunaendeleya kuomba kusudi mupate kutambua mapenzi yake katika akili na usikilivu wa kiroho . 10 Tunaendeleya tena kuomba kusudi mutembeye kama inavyomupendeza Bwana ,tena muzae matunda kwa kila tendo nzuri na mukomale katika ufahamu wa Mungu . 11 Tunaomba kusudi muwe na nguvu katika yote,kwa uwezo wa utukufu wake,katika utii na utulivu. 12 Tunaomba kusudi muwe na furaha ya kumushukuru Mungu aliyewapatia uwezo wa kurithi sehemu ya waamini katika nuru . 13 Alituokowa kutoka ufalme wa Giza,na kutupeleka katika ufalme wa mtoto wake mpendwa. 14 Tulikombolewa na kusamehewa zambi zetu, kupitiya mtoto. 15 Mtoto ni mufano wa Mungu asiyeonekana. Ni wa kwanza katika vyumbe vyote. 16 Kwa sababu kupitiya yeye vitu vyote viliumbwa, vyenye kuwa mbinguni na vyenye kuwa duniani , vinavyoonekana na visivyoonekana. Hata ikawa Enzi, heshima, utawala ao uwezo, vyote vimeumbwa na yeye na kwa ajili yake. 17 Yeye alikuwa mbele ya vitu vyote na vitu vyote viliumbwa na ye. 18 Yeye ni kichua cha mwili, yaani kanisa. Naye ni mwanzo, na wa kwanza katika wafu; Anakamata nafasi ya kwanza katika vitu vyote. 19 utimilifi wa yote unajulikana ndani yake. 20 Ilipendeza Mungu kurudisha masikili zano ya watu na Mungu kupitia mwana wake. kwa damu iliomwangika kwa musalaba ikalate uhuru kutoka kwa utumwa ya zambi Mungu alipatanisha mbingu na dunia. 21 Nyinyi pia wakati mmoja mulikuwa wageni na adui wa Mungu, kwa mawazo na matendo yenu mbaya. 22 Sasa kupitiya kifo chake anawapatanisha na mwili wake. Alifanya hivi kusudi muwe watakatifu, wasiyokuwa na dowa wala hatiya mbele yake. 23 Muwe na misingi katika imani na musitingizike, na musitoke katika tumaini mulilo nalo katika habari njema luliyo sikiya. Na ni hii habari njema ilyo hubiriwa kwa watu wote duniani. Na kupitiya hii habari njema njo mimi Paulo ninakuwa mutumishi. 24 Sasa nafurahi katika mateso yangu ajili yenu. ninalipa deni ya tabu ya juu ya mapendo aliyo nayo kuhusu mwiliwake, kanisa. 25 Ni juu ya ile kanisa njoo niko mtumishi sawa na kazi niliyopewa na Mungu, juu ya kutimiza maandiko. 26 Hii ndiyo siri ya ukweli uliyofichwa toka vizazi vya zamani, sasa inafunuliwa kwa wale waliyo muamini. 27 Alipenda kuonesha utajiri wa siri ya utkufu katikati ya wapagano. Ni kusema Kristo yuko kwenu tumaini ya utkufu utakaokuja 28 Ni yeyé tunayehubiri. Tunashauriya na kufundisha watu wote katika akikili, kusudi tupeleke watu wote wakiwa wanakamilika katika Kristo. 29 Kwa sabu hii ninatumika na kupigana kupitiya nguvu na uwezo aliyo tiya ndani yangu.