Sura 17

1 Jamii yote ya Israeli ili safiri kutoka nyikani ya Sini, wakifuata maelekezo ya Yahweh. Walieka kambi Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa. 2 Hivyo watu wakamlaumu Musa kwa hali yao na kusema, "Tupe maji ya kunywa." Musa akasema, "Kwanini mnagombana na mimi? Kwanini mnajaribu Yahweh?" 3 Watu walikuwa na kiu sana, na waka mlalamikia Musa. Wakasema, "Kwa nini umetutoa Misri? Ili utuue sisi na watoto wetu na mifugo yetu kwa kiu?" 4 Kisha Musa akamlilia Yahweh, "Nini nimefanya kwa hawa watu? Wako tayari ata kunipiga mawe." 5 Yahweh akamwambia Musa, "Nenda mbele yao, na uchukue baadhi ya wazee wa Israeli. Chukua gongo ulilo piga nalo mto, na uende. 6 Nitasimama mbele yako pale kwenye mwamba wa Horebu, na utaupiga mwamba. Maji yatatoka ya watu kunywa." Kisha Musa akafanya hivyo mbele ya wazee wa Israeli. 7 Aliita ile sehemu Massa na Meriba kwa sababu ya malalamishi ya Waisraeli, na kwa sababu walimjaribu Bwana kwa kusema, "Je Yahweh yupo miongoni mwetu au hapana?" 8 Kisha jeshi la watu wa Ameleki wakaja na kushambulia Israeli huko Refidimu. 9 Hivyo Musa akamwambia Yoshua, "Chagau wanaume kadha na uende nje. Pigana na Ameleki. Kesho nitasimama juu ya kilima na gongo la Mungu mkononi mwangu." 10 Hivyo Yoshua akapigana na Ameleki kama Musa alivyo elekeza, wakati Musa, Aruni, na Huri walienda juu ya kilima. 11 Wakati Musa alipokuwa ameshikilia mikono yake juu, Israeli ilikuwa yashinda; alipoacha mikono yake ipumzike, Ameleki alianza kushinda. 12 Mikono ya Musa alipokuwa mizito, Aruni na Huri walichukua jiwe na kuweka chini yake alikalie. Muda huo huo, Aruni na Huri walinyanyua mikono yake juu, mtu mmoja upande mmoja, na mtu mmoja upande mwingine. Hivyo mikono ya Musa ilishikiliwa tuli mpaka jua lilipo zama. 13 Hivyo Yoshua akawashinda watu wa Ameleki kwa upanga. 14 Yahweh akamwambia Musa, "Andika haya kwenye kitabu na umsomee Yoshua, kwa sababu nitaondoa kumbukumbu ya Ameleki kutoka chini ya mbingu." 15 Kisha Musa akajenga madhabahu na kuiita "Yahweh ni bendera yangu." 16 Alisema, "Kwa kuwa mkono ulinyanyuliwa juu kuelekea kiti cha enzi cha Yahweh - kwamba Yahweh atafanya vita na Ameleki vizazi na vizazi."