Sura 15

1 Kisha Musa na watu wa Israeli wakaimba huu nyimbo kwa Yahweh. Waliimba, "Nitaimba kwa Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu; farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari. 2 Yahweh ni uweza wangu na nyimbo zangu, na amekuwa wokovu wangu. Huyu ni Mungu wangu, na nitamsifu, Mungu wa baba yangu, nitamtukuza. 3 Yahweh ni shujaa; Yahweh ni jina lake. 4 Ametupa magari ya farasi. ya Farao na jeshi lake kwenye bahari. Maafisa wa Farao hodari walizama kwenye Bahari ya Shamu. 5 Kina kiliwafunika; walienda kwenye kina kama jiwe. 6 Mkono wako wa kulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu; mkono wako, Yahweh, umewavunja adui. 7 Kwa utukufu mkubwa umewapindua walio inuka dhidi yako. Umetuma gadhabu; imewateketeza kama karatasi. 8 Kwa pumzi ya pua yako maji yalio jaa; maji yanayo tembea yalisimama wima na kujaa juu; maji yalikuwa manene ndani ya kilindi cha bahari. 9 Adui alisema, 'Nitakimbiza, nitapita, nitagawa nitakacho chukua; tamanio langu litatimizwa kwao; nitavuta upanga wangu; mkono wangu utawaharibu wao.' 10 Lakini ulipuliza kwa upepo wako, na bahari ikawafunika wao; walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi. 11 Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu? Nani kama wewe, mtakatifu wa utukufu, katika sifa umetukuzwa, anaye fanya miujiza? 12 Ulinyoosha mkono wako wa kulia, na dunia ikawameza. 13 Katika uaminifu wa agano lako umewaongoza watu ulio waokoa. Katika uweza wako, umewaongoza katika sehemu takatifu unayo ishi. 14 Watu watasikia, na watatetemeka; hofu itawakumba wakazi wa Filistia. 15 Kisha wazee wa Edomu wataogopa; wanajeshi wa Moabu watetemeka; wakazi wote wa Kanani watayeyuka. 16 Mshituko na hofu vitawaangukia. Kwa sababu ya nguvu ya mkono wako, watakuwa kimya kama jiwe hadi watu wako watakapo pita, Yahweh - hadi watu ulio waokoa watakapo pita. 17 Utawaleta na kuwapanda kwenye mlima wa urithi wako, sehemu, Yahweh, ulio jenga ya kuishi, sehemu takatifu, Bwana wetu, mikono yako iliyo jenga. 18 Yahweh atatawala milele na milele." 19 Kwa kuwa farasi wa Farao walienda na magari ya farasi na wapanda farasi kwenye bahari. Yahweh alileta maji ya bahari juu yao. Lakini Waisraeli walienda juu ya nchi kavu katikati ya bahari. 20 Miriamu nabii wa kike, dada wa Aruni, akanyanyua tari, na wanawake wote wakatoka na matari, wakicheza naye. 21 Miriamu akawaimbia: "Muimbieni Yahweh, kwa kuwa ameshinda kwa utukufu. Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini. 22 Kisha Musa akaongoza Israeli mbele kupita Bahari ya Shamu. Walienda nyikani ya Shuri. Walisafiri kwa siku tatu nyikani pasipo kuona maji yeyote. 23 Kisha wakaja Mara, lakini hawakunywa maji ya huko kwa sababu yalikuwa machungu. Hivyo wakaita hiyo sehemu Mara. 24 Hivyo watu wakamlalamikia Musa na kusema, "Nini tunaweza kunywa?" 25 Musa akamlilia Yahweh, na kumuonyesha mti. Musa akautupa kwenye maji, na maji yakawa matamu kunywa. Ndio pale Yahweh alipowapa sheria kali, na ndio pale alipo wajaribu. 26 Alisema, "Kama utasikiliza sauti ya Yahweh Mungu wako kwa umakini, na kufanya yalio sahihi machoni pake, na kama utatega sikio kwa amri zake na kutii sheria zake zote - sitawaletea ninyi magonjwa yale niliyo waletea Wamisri, kwa kuwa mimi ni Yahweh ninaye kuponya." 27 Kisha watu wakaja Elimu, palipo kuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mtende. Waliweka kambi hapo pembeni mwa maji.