Sura 4

1 Nabukodonozori mufalme, kwa batu bote, ma taifa yote na kwa batu ba kila luga benye bana ishi mu dunia yote. Mupate amani kwa uwingi! 2 Nili pendelea ni julishe alama na maarifo yenye Mungu mukubwa ame ni tendea. 3 Vile alama ziko kubwa kweli! ile maarifa ni za nguvu kabisa! ufalme yake ni ya milele, na utawala yake ina dumu bizazi hata bizazi. 4 mimi Nabukodonozori, nilikua na ishi mu nyumba yangu salama na raha mu nyumba yangu ya kifalme. 5 Nili pata ndoto ye iliniogopesha; mawazo yenye ilinifutilia mu kitando yangu, na maono ya moyo yangu ilikua na ni letea boga muakali. 6 Nili toa oda balele batu ya hekima ba babiloni bote kusudi bampe mafasirio ya ndoto. 7 Halafu bachawi, batu ya akili, bakalidayo, na bagaga bakakuya. Nika baambia ndoto lakini habakuni patia mafsaio yake. 8 Kwa mwisho, ba nitetea Danieli mwe anaitiwa Baltari kulingana na jina ya mungu wangu, ye njo ali kwa na roho ya Mungu mutakatifu ndani yake nika muambia ndoto: 9 Baltazari, kiongozi ya bachauvi wenjo uko na roho ya Mungu mutakatifu mina jua, hakuna siri ya ku mushinda nguvu, nipatie ma fasirio ya maana yenye niliona mu ndoto. 10 Maona ya moyo yangu njo hii, wakati nilikua na lala niliona katikati ya dunia kulikua muti murefu saana. 11 Ile muti ikakua mukubwa na nguvu saana, kipande yake ya juu ili inuka mpa mu mawingu na pande zote za dunia bali iona. 12 Majani yake ilikua muzuri, na matunda yake ilikua mingi sana. Ili patia batu bote chakula, nyama za pari zili jifichi chini ya kivile yake, ngege za anga zili ishi mu matawi yake, na kila mweye uhai alipata chakula kwake. 13 Mu maono ya moyo yangu, yenye nili ona mukitanda yangu, nili angalia, na tazama mumoja wa bale benye kukesha na batakatifu bakashuka toka mbinguni. 14 Aka sema na sauti kubwa: mukate muti, na mukatekete matawi yake, mukungute ma yani yake, na sambaraze matunda, ma myama yote ikimbie chini yake, na ma ndege zi kimbie matawi yake! 15 Lakini muache kipande yenye kua na mi zizi mu bulongo kisha mifunge na mikufu ya chuma na shaba, katiakati ya ma yani ya mu shamba. Ilobane na umande ya mbingu na ipate kula mayani kama nyama. 16 Roho yake ya kimutu itamuloka, na atapata roho ya myama, na nyakati saba zita pita na iko mwa ile hali. 17 Ile hukumu ni ya siri ya benye kukesha, ile hatua ni oda ya bata katifu, kusudi benye nzima bajue kama wajuu sana anatawala yulu ya ma ufalme ya batu, na ana bapanaka kwa mwenye ana furahia na anainu botu benye nguvu. 18 Ile njo ndoto yenye nili pata mimi mufalme Nabukodonozori, muipatee mafasirio sababu batu bahekima ba mu ufalme na bawezi kuni patia nayo; weye una iweza sababu ndani yako, uko na roho ya Mungu mtakatifu. 19 Halafu Danieli, mwe aliituwa Baltazari, aka pata mushangao kwa muda, na mawazo yake ilimu vuruga. Mufalme akasema tena Baltazari, ndoto na mafisirio yake isiku vuruge akili! Baltazri aka jibia. Bwana yangu, ile ndoto ikue ata ya ba adui bako, na mafasirio yake ikue ata ya bapinzanibako! 20 Mutu yenye uli ona, yenye ilikua mukubwa na ya nguvu, nikusema kipande ya juu ili panda mpaka mu mawingu na yenye bali ona pande zote za dunia. 21 Ile muti yenye mayani ilikua muzuri na matunda kwa wingi, na ili patia batu yote chakula, na ba nyama bote ba pori bali fichama mu kwili yake na mu matawi yake ba ndege ilishi amo. 22 Ni weye Ee mufalme wenjo ulisha kua mukubwa na wa nguvu, ni kusema bikuwba yako ili panda mpaka mbinguni na mamulaka yako ina kamata pande zote za dunia. 23 Mufalme aliona mu mojo mu benye kukesha na batakatifu iko nashuka taka mbinguni ana sema: mukale muti, na mu harribishe lakini mwache shina mu bulongo kwenye mizizi iko, na muifunge na mikufu zo chuma na shaba, na chakula yake ai ohangie na ba nyama ya mu pori mpaka ma wakati saba zimu pilie mua ile hali. 24 Mafasirio njo hii Ee mufalme, tazama siri na oda ya ule mwenye iko yulu zaidi yenye itati milika ju yako. Ee mufalme. 25 Bata kufukuzaka mu batu, uta pata makao pamoja na ba nyama ya pori, bata kua na kupatia mayani ukule sawa ngombe, uta lobana na umande wa mbingu, ma wakali saba zipite na uko mwa ile hali, mpaka ujue kama mwenye iko yulu sana ana tawala ju ya ma ufalme zote za batu na anazi pana kwa mwenye ana taka. 26 Oda ya acha shina ya muti kwenye mizizi iko ni kusema kama ufalme yako itabakia mapka siku uta tambuo kama mwenye kuta wala iko mbinguni. 27 Njo mana Ee mufalme, hii shauri yangu ikupendeze, uache zambi zako utende haki, na uacha mabaya yako usikilie bazaifu uruma, na raha yako ita endelea. 28 Ile yote inatimilikia ju ya mufalme Nabukodozori. 29 Nyama ya myezi kumi na mbili, alikua na ji tembeza mu nyumba ya kifalme huko Babiloni, 30 Mufalme akasema, hapa haiko Babiloni mukubwa, yenye nili jengaka, sawa makao ya kifalme, kwa uwezo ya nguvu yangu na ju ya utukufu ya enzi yangu? 31 Kauli ilikua ikingali mukinywa ya mufalme, sauti ikashuka toka mbinguni: sikia mufalme Nabukodonozori bata ku nyanganya ufalme. 32 Bataku fukuza katikati ya batu, uta na makao na ba nyama ba mu pori, bata ku patia mayani ukule sawa ngombe, na nyakati saba zita pita na uko mwa ile hali mpaka uta tambua kama mweniko juu sana, anatawala ju ya ufalme ya batu na anaipatia mwenye ana taka. 33 Pale pale ile neno ika timilika ju ya Nabukodozori. Aka fukuziwa mu katikati ya batu, akakula mayani kama ngombe, mwili yake ika lobana umande ya mbinguni, mpaka nywele zake zika refuka sawa manyoa ya tai, na makucha yake kama ya ndege. 34 Kisha muda yenye ili wekwa, miye Nabukodozori, nili inua macho mbinguni, na ufalme ika ni rudilia. Nikabariki [Mungu] wa juu sana, nika sifu na kuabudu mwenye maisha ya milele na uta wala yake ni ya milele, na ufalme yake ina dumu vizazi hata vizazi. 35 Bakaaji bote ba dunia biko bure mu macho yake; ana tenda gisi ana penda na jeshi la mbinguni pia na bakaaji ba ba mu dunia, na hakuna mutu mwenye anabakia kwa mukono ya mwene ana weza ku muuliza: una fanya nini? 36 Mwa ile wakati, ufahamu ika nirudilia, utukufu ya ufalme yangu, na enzi yangu na nika pata tena ku meremela yangu, bashauri na batu bangu bakubwa baka ni hitaji tena, nika rudishiwa, ufalme yangu baka inirudishia tena na mamtaka yangu ika rudia tena. 37 Sasa mie Nabukodozori, mina ninasifu, nainua, na tukuza mufalme wambingu, mwenye matendo yake ni ya kweli na njio za haki, na ye njo anaweza shusha benye bana tembea na majivino.