1 Mu mwaka ya pili ya utawa la ya Nabukodonozori, Nabukodonozori aka leta ndoto. Roho yake ili babaika, na haku pata busingisi. 2 Mufalme akaitisha, banganga, batu ya akili, wachawi, na wa kalidoyo kusudi ba mwambie ndoto zake, bakakuya na ba kajionesha mbele ya mufalme. 3 Mufalme akabaambia, nilipata ndoto, roho yangu inababaika na nili taka kujua ile ndoto. 4 Wakalidayo waka mujibu mufalme mu luga ya kiaramia. Ewe mufalme, nishi milele, uwa ambie batumishi yako ile ndoto na shie tuta leta mafasirio. 5 Mufalme aka kamata tena neno aka sema: Jambo imenipotea, kama hamuni julishe ndoto na mafasitio yake, muta katwakatwa bipande bipande, na nyumba zenu zita geuka na yalala. 6 Lakini muki niambia ndoto na mafasirio yake muta pata kwangu mazawadi na bitu pia na heshima kubwa. Njo kwa mana muniambie ndoto na mafasirio yake. 7 Baka jibu mala ya pili: Mufalme aambie batumishe yake ile ndoto na shie tulete mafasirio. 8 Mufalme aka kamata neno akasema: Mina gundua kwa kweli kama munapenda kuchukua muda ju munaona kama ile kitu ina pitia. 9 Kama hama ni julishe ndoto, ile hukumu ita ba kamata nyi bote, muna taka ji andaa kuniambia bongo na budanganyifu, kwa kungozea muda ibadilike. Njo mana [mina sema] muni julishe ndoto na mi nta jua kama muko na uwezo ya ni patia maana yake 10 Bakalidayo ba jibia mufalme hakuna mutu [hapa] ku dunia mwenye an weza kusema byenye mufalme ana lomba na hakuna mufalme ata angekua mukubwa wala mwenye nguvu ya mamuna gani mwenye alishaka shurutisha kitu ya vile kwa muchawi, muakili wala mukalideo yeyote. 11 Byenye mufalme analomba ni bya nguvu, hakuna mutu mwenye ana wezi kwambia mufalme, kama haiko Mungu tu, mwenye makao yake haiko mu batu. 12 Mufalme aka kasiruka pale pale na ku huzu nika, na ku toa oda kama baue bale bazee bote ba Babiloni. 13 Hukumu ika tangazwa na bakawa bale bazee bote kisha ba kaanza kutafuta Danieli na Benzake kusudi babaue nabo babaue. 14 Halafu Danieli akauliza na Harjoki mukubwa wa Balinzi ya mufalme: mwe alitoka kwenda kuanganiza na kuua bale bazee ba Babiloni. 15 Akaambia Harjoki kioogozi wa [ma jeshi] ya mufalme ju ya nini malipizi ya mufalme ni ya makali vile? Harjoki [akaanza] kumu elezea. 16 Njo Danieli akaendea, mufalme na aka mu bembeleza [kusudi] amupe tena muda ya ku muletea ma fasirio. 17 kiisha Danieli akaenda kwake ku nyumba, na ku wa arifu Hanania, Mikaeli na Azaria kwa ile maneno. 18 Aka bapatia kazi ya kuomba rehema ya Mungu wa mbingu, na njo Danieli na benzake pia na baze benye bali bakiaka mu Babiloni. 19 Sisi ikafunuliwa kwa Danieli mumaono busiku na Danieli aka sifu Mungu wa mbingu. 20 Danieli aka kamata neno, aka sema libarikiwe jina la Mungu milele na milele, yeye njo iko na hekima na nguvu. 21 Ni yeye njo anabadilishaka nyakati na majira anapinaua na ye njo ana wekaka biongozi [bafalme] ana patiaka batu ya hekima busara na ujuzi kwa benye biko na akili. 22 Ana ifunula byakindani byenye bina fichikiwa, ona jua byenye biko mugiza, na mwangaza ina ikalaka naye. 23 Mungu wa ba babu yangu, nina ku inua na nina kusifu, kuona ulinipa hekima na nguvu na kwa sababu ume ni julisha byenye tuli kulomba na kutu funulia siriya mufalme. 24 Kisha ile, Danieli akaenda kwa Harjoki mwenye mufalme alipatiaka oda ya kutegeteza batu ya hekima bote ba Babiloni, unipeleke kwa mufalme ni mupatie ma fasirio. 25 Harjoki aka mupeleka Danieli pale pale mbele ya mufalme naye akamwambia hivi, mu ba mateka ba Yudea, nilipata mutu moja mwenye ata patia mufalme mafasirio. 26 Mufalme akauliza Danieli mwe alikuaka naitwa Belitazari: weye uko na uwezo ya kuni niambia ndoto ni pata na mafasirio yake? 27 Danieli akajibu mbele ya mufalme akasema: yenye mufalme analomba ni siri yenye batu ya akili, bagnga na bachawi na bana uwezo ya kuifafnulia mufalme. 28 Lakini kule juu mu mbingu kuko Mungu moja mwenye ana funulaka ma siri, na alijulisha kwa mufalme Nabukodonozori byenye bitafika mu kisha muda [fulani] ndoto yake yenye uliona wakati ulikua na lala njo hiyi 29 Mu busingizi, Ee mufalme, mawazo yenye kugusia byenye bitakua kisha hii wakati, na mwenye ana funulaka ma siri ali ku julisha byenye bita fikaka. 30 Kama nili funuliwa ile siri, haiko juu niko na hekima kushinda batu bote benye ku pumua, lakini ni kusudi mufalme apale mafa sirio na ujue mawazo ya moyo wako 31 Ee mufalme ulikwa na tazama na uliona sana mu kabambi, ile sanomu ilikua kubwa kabisa na ilikua angaro kimaajabu, ilikua na simama mbele yako na hali yake ilikua ya kuogopesha. 32 Kichwa ya ile sanamu ilikua ya zahabu safi, kifua yake na mikono yake ilikua ya zahabu, tumbu yake na ma paja yake ilikua ya shaba; 33 Migulu yake ilikua ya chuma milundi yake kipande ilikua ya chuma na kipande ingine ya bulongo. 34 Ulikua na angalia wakati lijiwe ilitoka yopeke bila kusukumwa, ikapiga ile migulu ya chuma na bulongo ya ile sanamu na ikaivunja vunja bipande bipande. 35 Ndipo ile chuma, bulongo, shaba, zahabu na feza, bika vunjika na kua kama kabumbu yenye ina panda mu hewa wakati ya kipwa, mupepeo ika bibeba na hakuna alam yabyo yenye ilionekana tena. Lakini lijiwe yenye ili piga sanamu ikakua mulima mukubwa, na ikataza dunia mzima. 36 Ile njo ndoto. Tutapatia mufalme mafasirioyake. 37 Ee Mufalme, uko mufalme sabau Mungu wa mbingu alikupatia, ufalme wa bafalme, mamulaka, nguvu na uwezo. 38 Alitia mu mikono yako maeneo fulani kwenye batu banaikala, nyamaza pori, na ndege za anga na alikufanya utawale bile byote, we njo uko kichwa ya zahabu 39 Nyuma yako ufalme ingine itainuka ya chinikushinda yako; Na ufalme ya tatu yenye ita kua ya shaba na itatawala dunia mzima. 40 Kutakuwa na ya ine, nguvu kama chuma, vile vile chuma ina vinjaka na kubomola kila kitu, nayo ita vunja na kubomola bitu yote sawa chuma yenye ina vunja -vunja bitu yote. 41 Na gisi uliona migulu ya chuma na bidolo ya kipande bulongo ya mufunyanzi na kipande chuma, ile mafalme yote ita gawanyika lakini kutakua nguvu ya chuma ndani yake sababu uliona chuma ina chonoana na bulongo. 42 Na gisi bidole ya migulu ilikua nusu chuma na nusu bulongo ile ma falme itakua nguvu kidogo na tegetege kidogo. 43 Uliona chuma inahangiwa na bulongo, sababu zitaji unga kwa mapatano za kibinadamu, lakini ha bata ungana huyu kwa mwenzake ni kama vile chuma haiwezi ungana na bulongo. 44 Wakati ya bale bafalme, Mungu wa mbingu ata inwa ufalme yenye haita, haribiwa, na haitapita chini ya uta wala wa ingine wa ingine taifa, ita vunja na kutegeteza zile ma falme zote na yo yenyewe ita dumu milele. 45 Ile njo ina fafanula lijue yenye uliona ina jitosha ku mulima bila musaada ya mukono ata moja na ika vunja chuma, shaba, bulongo, feza na zahabu. Mungu mukubwa ali julisha mufalme byenye bita fika nyuma ya ile. Ndoto ni ya kweli na mafasirio yake ni hakika. 46 Halafu mufalme aka anguka kwa uso wake na kuinama mbel ya Danieli, na aka toa oda kwamba ba mutolee zabihu na manukato. 47 Mufalme aka ambia Danieli, kweli Mungu wako ni Mungu wa miungu yote na Bwana wa bafalme, na an funuluka masiri sababu uliweza kugundua siri. 48 Kisha mufalme akainua na kumupatia matabishi na bitu mingi, aka mupa uongozi ya ma jumbo zote za Babiloni, na ku mu simika kiongozi mukubwa wa bazee bote ba Babiloni. 49 Danieli akaomba mufalme atie Shadraki, Meshaki na Abed Nego kusimamia jumbo la Babiloni, na Danieli akabakia mu baraza ya mufalme