Genesis 11

Genesis 11:1

Mara baada ya gharika, kulikuwa na lugha ngapi juu ya uso wa nchi yote?

Mara baada ya gharika, kulikuwa na lugha moja juu ya nchi yote.

Kwa nini watu walijenga mji na mnara wao?

Watu walijenga mji wao na mnara katika nchi ya Shinari.

Genesis 11:3

Watu waliamua kufanya nini badala ya kusambaa juu ya nchi yote kama vile Mungu alivyowaamuru?

Badala ya kusambaa juu ya nchi yote kama vile Mungu alivyoamuru, watu waliamua kujenga mji na mnara.

Watu walitaka kutengeneza nini kwa ajili yao wenyewe?

Watu walitaka kujitengenezea jina kwa ajili yao.

Genesis 11:5

Yahwe alishuka chini kufanya nini kwa watu?

Yahwe alishuka chini na kuchanganya lugha ya watu.

Kwa nini Mungu alifanya hivi?

Mungu alichanganya lugha zao ili wasiweze kuelewana wao kwa wao.

Genesis 11:8

Mungu alisababisha nini kwa watu kufanya?

Mungu alisababisha watu kusambaa juu ya uso wa nchi yote, kama alivyokuwa ameamuru.

Jina la mji ambao watu walijaribu kujenga ulikuwa unaitwaje?

Jina la mji ulikuwa Babeli.

Genesis 11:10

Ni vizazi wa mwana yupi wa Nuhu wanapewa katika sura hii?

Vizazi vya Shemu, mwana wa Nuhu, wanapewa katika sura hii.

Genesis 11:24

Nani alikuwa baba wa Abramu?

Baba wa Abramu alikuwa Tera.

Genesis 11:27

Mwana wa Tera Harani alikuwa na mwana mwenye jina gani?

Mwana wa Tera Harani alikuwa na mwana aliyeitwa Lutu.

Tera alikuwa akiishi wapi?

Tera aliishi Uru miongoni mwa Wakaldayo.

Genesis 11:29

Jina la mke wa Abramu lilikuwa nani?

Mke wa Abramu alikuwa akiitwa Sarai.

Mke wa Abramu alikuwa na tatizo gani?

Mke wa Abramu Sarai alikuwa tasa na hakuwa na watoto.

Genesis 11:31

Tera alihama pamoja na Abramu, Sarai na Lutu kwenda wapi?

Tera alihama katika nchi ya Kaanani pamoja na Abramu, Sarai na Lutu.