Genesis 5

Genesis 5:1

Sura ya tano ya Mwanzo ni kumbukumbu ya nini?

Sura ya tano ya Mwanzo ni kumbukumbu ya vizazi vya Adamu.

Binadamu aliumbwa katika mfano wa nani?

Binadamu aliumbwa katika mfano wa Mungu.

Mungu aliumba binadamu wa jinsia gani?

Mungu aliumba binadamu wa kiume na kike.

Genesis 5:3

Adamu aliishi muda gani?

Adamu aliishi miaka 930.

Genesis 5:6

Sethi aliishi muda gani?

Sethi aliishi miaka 912.

Genesis 5:12

Kenani aliishi muda gani?

Kenani aliishi miaka 910.

Genesis 5:18

Yaredi aliishi muda gani?

Yaredi aliishi miaka 962.

Genesis 5:21

Mahusiano ya Henoko na Mungu yalikuwaje, na nini kilitokea kwake?

Henoko alitembea na Mungu, na Mungu akamtwaa.

Genesis 5:28

Lameki alisema nini kuhusu mwanawe Nuhu?

Lameki alisema ya kwamba Nuhu atawapa wanadamu pumziko kutoka kwa kazi na taabu iliyosababishwa na ardhi ambayo Mungu aliilaani.

Genesis 5:32

Wana wa Nuhu walikuwa kina nani?

Wana wa Nuhu walikuwa Shemu, Hamu, na Yafethi.